Instagram

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, May 25, 2017

MANCHESTER UNITED NDIO MABINGWA WAPYA WA UEROPA







Thursday, December 12, 2013

Mandela aivuta dunia kuhamia Afrika Kusini


Mashada na Picha ya Rais mstaafu wa Afrika Kusini Marehemu Nelson Mandela anayetarajiwa kuzikwa jumapili ya tarehe 15 Disemba, 2013  


Johannesburg. Viongozi zaidi ya sabini wakiwamo wakuu wa nchi na Serikali wanatarajiwa kushiriki hatua mbalimbali za safari ya mwisho ya Mzee Mandela aliyefariki Alhamisi ya Desemba tano usiku.
Anatarajiwa kuzikwa Jumapili ijayo, Desemba 15, 2013 katika Kijiji cha Qunu alikokulia, mazishi ambayo yanatarajiwa kuwavuta maelfu ya watu kutoka kona mbalimbali za dunia.
Hata hivyo hadi jana maofisa wa Serikali ya Afrika Kusini walisema walikuwa bado hawajapata orodha kamili ya viongozi wote watakaohudhuria, l pia wakashindwa kusema iwapo Rais Obama atakwenda Qunu au atashiriki katika hatua nyingine za awali za msiba huo kabla ya mazishi ya Jumapili.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani, Jay Carney alinukuliwa akithibitisha kwamba Obama na mkewe Michele watashiriki katika msiba huo lakini hakuwa tayari kueleza suala hilo kwa undani. Habari zaidi zilizopatikana jana mjini Johanesburg zinasema Rais wa Brazil, Dilma Rousseff atakuwa miongoni mwa wageni mashuhuri watakaoshiriki.
Balozi wa Marekani nchini Afrika Kusini, anasema kuwa: “Rais Obama, amethibitisha kushiriki mazishi ya Madiba” (akirejea) jina maarufu la Mzee Mandela, taarifa ambayo ilitiliwa na nguvu na habari zilizoinukuu Ikulu ya Washington ikithibitisha ujio wa kiongozi huyo pamoja na watanguliza wake; George W. Bush na Bill Clinton.
Vyombo mbalimbali vya habari vilinukuu taarifa ya Ikulu ya Marekani ikisema: “Rais Obama na mkewe watakwenda Afrika Kusini wiki ijayo kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa ajili ya kumbukumbu ya Nelson Mandela na watashiriki katika tukio hilo la kukumbukwa.”
Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma alitangaza ratiba ya maombolezo ya shujaa huyo aliyeongoza vita dhidi ya sera za ubaguzi wa rangi zilizokuwa zikitekelezwa na Makaburu na jana ilikuwa ni siku ya maombi ya kitaifa kwa ajili ya Mzee Mandela.
Leo Jumanne kutakuwa na tukio la kitaifa katika Uwanja wa Michezo wa FNB, Johannesburg ambako ni sehemu ya hitimisho ya safari ya Mandela huku watu zaidi ya 80,000 wakitarajiwa kuhudhuria na kati ya kesho Jumatano na Ijumaa, mwili wa Mandela utakuwa katika Majengo la Umoja (Union Buildings) Pretoria ambako utaangwa kwa siku tatu mfululizo.
Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Afrika KusiniNeo Momodu aliwaambia waandishi wa habari jijini Johannesburg kuwa watuwa Pretoria watakuwa na nafasi ya kushuhudia mwili wa Mandela ukisafirishwa kutoka chumba cha kuhifadhia maiti kwenda Jengo la Umoja kila asubuhi kwa siku tatu mfululizo.
Momudu anasema mitaa ambayo mwili huo utakuwa ukipitishwa itatangazwa ili kuwezesha wakazi wake na wananchi wengine kupata fursa ya kujipanga pembezoni mwake kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa kiongozi huyo.
“Njia ambazo mwili wa marehemu utakuwa ukipitishwa kila asubuhi kutoka chumba cha kuhifadhia kwa ajili ya kupelekwa kupewa heshima za mwisho, zitatangazwa na tutawaomba wananchi kujipanga pembezoni mwa njia hizo wakati mwili huo ukipita katika mitaa hiyo ya Pretoria,” anasema.
Hata hivyo, Momodu anasema utaratibu wa kutoa heshima za mwisho utaratibiwa na kuna uwezekano mkubwa kwamba si kila mtu atakayeweza kuingia katika eneo hilo na kwamba kila mmoja atakayeingia lazima awe na kitambulisho maalumu.
 Anasema kutakuwa na eneo maalumu la kusubiri kuingia kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho na kwamba watakafanikiwa kupata ruhusa ya kwenda kuaga, watakuwa wakipakiwa kwenye mabasi maalumu yaliyoandaliwa kwa ajili ya kazi hiyo na watarejeshwa na mabasi hayo.
Jumamosi, Desemba 14, mwili wa Mandela utasafirishwa kwenda Qunu ambako Jumapili Desemba 15, utazikwa rasmi.

Friday, August 30, 2013

LEO NDIO LEO CHEKA VS WILLIAMS.

b
Bondia Francis Cheka (kushoto) na Phil Williams kutoka Marekani, kwa pamoja wakiwa wameshika Taji la Ndondi la Dunia (WBF) mara baada ya kumaliza kupima uzito katika  Ukumbi wa Idara Habari Maelezo jana, tayari kuzikunja leo kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam. Picha na Michael Matemanga. 
Dar es Salaam. Bingwa wa Masumbwi, Francis Cheka amesema dhamira ya kumtandika mpinzani wake, Phil Williams kutoka Marekani katika pambano lao usiku wa leo, iko palepale.
“Siwezi kumwangusha Rais Jakaya Kikwete, namwahidi nitashinda mchezo wa leo na kuubakisha mkanda wa ubingwa Tanzania,” alisema Cheka wakati akiongea na Mwananchi jana.
Cheka anashuka ulingoni, Diamond Jubilee kuzikunja na Williams katika pambano la kuwania Ubingwa wa Dunia (WBF), huku Makamu wa Rais, Gharib Bilal akiwa mgeni rasmi kumwakilisha Kikwete.
Mabondia hao, jana walipima uzito jijini Dar es Salaam tayari kwa pambano hilo linalosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa ndondi nchini.
“Najua JK (Jakaya Kikwete) ni mpenda michezo na anatoa sapoti kwenye michezo, hivyo namwahidi kufanya kweli leo,” alisema Cheka na kuongeza: “Nimejipanga kushinda pambano hili, nilishasema tangu awali, narudia kusema tena, sitawaangusha mashabiki wangu.”
Aliongeza: “Niko tayari kufia uwanjani, lakini siyo kuliona taji linaondoka Tanzania. Nitamaliza kazi kwa mafanikio.
Kwa upande wake, Williams alisema amekuja kushindana na siyo kinyume chake, hivyo anajiandaa kutoa upinzan mkali dhidi ya mpinzani wake.
Mwanamasumbwi huyo anashuka dimbani ikiwa ni wiki mbili kupita tangu amshinde kwa pointi bondia wa Malawi, Chiotcha Chimwemwe. Pia kutakuwa na mapambano ya utangulizi kati ya Thomas Mashali na Mada Maugo watakaowania Ubingwa wa WBF Afrika.

Eto'o asaini mkataba na Chelsea

Samuel Eto'o
Chelsea imemsajili mshambuliaji wa Cameroon, Samuel Eto'o kutoka klabu ya Anzi Makhachkala ya Urussi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka thelathini na miwili amesaini mkataba wa mwaka mmoja na Chelsea.
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho, aliamua kumsajili Eto'o baada ya maombi yake ya kumsajili nyota wa Manchester United Wayne Rooney kukataliwa.
Mapema wiki hii, ilibainika kuwa Rooney hakuwa tayari kulazimisha uhamisho wake kwa kuwasilisha ombi lake la kutaka kuondoka na hivyo kuzima matumaini ya Chelsea ya Kumsajili mchezaji huyo.
Mchezaji huyo ambaye ni mshindi mara nne wa mchezaji bora wa soka barani Afrika, alikuwa nyota wa AC Milan mwaka wa 2010 wakati Mourinho alipoiongoza kushinda kombe la klabu bingwa barani Ulaya.
Mwaka wa 2011, Eto'o alivunja rekodi ya kuwa mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi duniani.
Klabu hiyo ya Anzi pia imemuuza kiungo wake Willian, mwenye umri wa miaka 25 kwa klabu ya Chelsea, baada ya mmiliki wa klabu hiyo mfanya biashara tajii Suleyman Kerimov kupunguza bajeti ya klabu hiyo.
Samuel Eto'o katika kikao na waandishi wa habari
Eto'o alianza kucheza soka ya kulipwa na klabu ya Real Madrid, lakini alisajiliwa na vilabu vya Leganes na Real Mollorca kwa mkopo kabla ya kupata mkataba wa kudumu Mallorca mwaka wa tisini na tisa.
Mchezaji huyo ambaye alikuwa katika kikosi cha Cameroon kilichoshinda kombe la mataifa ya Afrika mwaka wa 2002, vile vile alishinda kombe la Copa del Rey, kabla ya kujiunga na klabu ya Barcelona mwaka wa 2004.
Akiwa katika uwanja wa Nou Camp, alishinda kombe la klabu bingwa barani ulaya mara mbili mwaka wa 2006 na 2009 na alifunga bao katika fainali hizo mbili pamoja na kushinda kombe la ligi kuu ya La Liga mara tatu.
Mwaka wa 20098, Barcelona iliilipa Inter Milan pauni milioni arubaini pamoja na mchezaji huyo ili kumsajili Zlatan Ibrahimovic na mshambuliaji huyo alifanikiwa kushinda kombe la klabu bingwa barani Ulaya kwa mara nyingine chini ya Uongozi wa Mourinho katika uwanja wa San Siro.
Alijiunga na klabu ya Anzi na ripoti zinasema kuwa alikuwa akilipwa £167,825 kwa wiki mwaka wa 2011

Wednesday, August 28, 2013

ROBERT WAPOTEEN PHOTO ALBUM


ROBERT WAPOTEEN & BAKARI MTEKUFA


TEAM KILA KITU

TEAM WAKALI WA MEDIA

TEAM RESEACHER


Posted by Picasa

Miaka 50 ya "I have a dream"

Martin Luther King

Imetimia miaka 50 tangu Martin Luther King alipotoa hotuba yake ya kihistoria. King aliyekuwa mwanaharakati wa kupigania haki za watu weusi Marekani, alizungumzia ndoto yake ya kuwa na nchi yenye usawa kwa wote.
"Nina ndoto kwamba siku moja watoto wangu wanne wataishi kwenye nchi ambapo hawatatathminiwa kulingana na rangi ya ngozi yao bali kulingana na tabia yao." Ilikuwa tarehe 28 Agosti mwaka 1963, pale ambapo Martin Luther King na maelfu ya Wamarekani weusi waliandamana mjini Washington kudai uhuru na haki sawa ya kupata ajira kwa watu weusi. King alikuwa miongoni mwa waandalizi wa maandamano hayo na mmoja wa watu waliotoa hutoba siku hiyo. Hotuba yake ya I have a dream - yaani nina ndoto - inaelezea mustakabali anaoutamani kwa nchi yake. Alitaka Marekani iwe na umoja na watu wasibaguliwe kwa sababu ya rangi ya ngozi yao.
"Hatuwezi kuridhika iwapo mtu mweusi kutoka Mississippi hana haki ya kupiga kura na mtu mweusi anayeishi New York haoni sababu ya kupiga kura," alisema King katika hotuba yake. Miaka hamsini baadaye, sehemu fulani ya ndoto ya Martin Luther King imetimia. Kwa mara ya kwanza Marekani inaongozwa na rais mweusi.
Ubaguzi bado tatizo sugu
Barack Obama ni rais wa kwanza mweusi wa MarekaniBarack Obama ni rais wa kwanza mweusi wa Marekani
Barack Obama leo ataongoza maadhimisho ya miaka 50 ya hotuba ya King. Atatoa hotuba kwenye jengo la kumbukumbu ya Lincoln mjini Washington - mahali pale pale ambapo King alielezea ndoto yake miaka 50 iliyopita.
Obama ameeleza kuwa mafanikio yake kama mwanasiasa mwenye mamlaka makubwa zaidi Marekani, yamejengwa juu ya misingi ya juhudi za Martin Luther King na wenzake. Anaamini kwamba asingekuwa rais wa Marekani leo, kama wanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi wasingekuwa tayari kuvumilia vitisho, mateso na hata kufungwa jela.
Hata hivyo, ubaguzi wa rangi bado ni tatizo sugu kwenye baadhi ya maeneo ya Marekani. Kisa cha kijana Trayvon Martin aliyepigwa risasi na Mmarekani mwenye ngozi nyeupe aliyehisi kuwa Treyvon ni kibaka kiliweka wazi kwamba bado yapo maoni potofu juu ya watu weusi. Suala lililozusha mjadala mkubwa zaidi ni kwamba aliyempiga risasi kijana huyo hakupewa hukumu yoyote mahakamani.
Sherehe za leo za mjini Washington zitahudhuriwa pia na marais wa zamani wa Marekani. Bill Clinton na Jimmy Carter ni miongoni mwa wale watakaotoa hotuba.

DOWNLOAD NEW SONG - Shebby Love ft Mabeste-Mapenzi Basi



Zimbabwe kujenga bustani ya kifahari

Bwawa la Victoria



Serikali ya Zimbabwe imetangaza mpango wa kujenga kivutio cha kitalii, "Disneyland in Africa" katika maporomoko ya maji ya Victoria ili kuimarisha secta ya utalii nchini humo.
Waziri wa utalii wa Zimbabwe Walter Mzembi ameiambia BBC kuwa serikali ya nchi hiyo itatumia dola milioni mia tatu kujenga bustani hiyo.
Serikali ya nchi hiyo inajaribu kufufua secta ya utalii iliyosambaratika kufuatia mzozo wa kisiasa uliodumu kwa takriban miaka kumi iliyopita na kushuka kwa dhamani ya safaru ya nchi hiyo.
Rais Robert Mugabe alichaguliwa kuhudumu kuwa rais wa nchi hiyo kwa muhula wa saba katika uchaguzi mkuu uliokamilika mwezi uliopita.
Lakini waziri huyo amesema, serikali yake haitategemea maporomoko hayo ya maji ya Victoria pekee, lakini amesema bwawa hilo linauwezo wa kuinua uchumi wa taifa hilo kwa kiasi kikubwa.
''Tunafikiria kuijenga bustani hiyo ili iwe sawa na bustani ya Disneyland nchini Marekani, na itajumuisha hoteli za kifahari, medani ya burudani, hoteli na vifaa vya kuandaa mikutano. Hii ndio maoni yetu na tunahitaji watu ambao wataweza kuiendesha'' Alisema waziri huyo.
Awali Mzembi aliliambia shirika la habari la serikali la nchi hiyo kwua serikali ya rais Robert Mugabe inadhamiria kuanzisha mfumo ambao utaruhusu soko huria katika secta ya mabenki nchini humo, ambapo watu ambao sio raia wa nchi hiyo wanaweza kufungua akaunti nchini humo.
Waziri huyo aliyasema hayo wakati wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu utalii unaoandaliwa kwa pamoja na Zimbabwe na Zambia.
Uamuzi huo wa kuipa Zimbabwe fursa ya kuandaa kongamano hilo la Umoja wa Mataifa, umeshutumiwa vikali na shirika la kutetea haki za kibinadam la Umoja huo, lililo na makao yake mjini Geneva, likadai serikali ya nchi hiyo inaendelea kukiuka haki za kibinadam na kuwa uchaguzi uliokamilika hivi majuzi haukuwa huru na wa haki.
Serikali ya Zimbabwe pia inapanga kupanua uwanja wa Ndege wa Victoria Fall, mradi ambao utagharimu dola milioni mia moja hamsini.
Katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza mwaka huu, secta ya utalii nchini humo ilikuwa kwa asilimia kumi na saba na ikiwa uthabiti wa taifa hilo utadumishwa secta ya utalii ina uwezo wa kuchangia pato la taifa hilo kwa asilimia kumi na tano.