Instagram

Wednesday, August 21, 2013

Marcelo ampania Neymar El Classico!


           


MADRID, HISPANIA

INGAWA wanacheza pamoja katika timu ya taifa ya Brazil, lakini beki wa kushoto wa Real Madrid, Marcelo amempania vilivyo staa mpya wa Barcelona, Neymar, wakikutana katika mechi ya El Classico.
Mechi hiyo imekuwa ikizua ukorofi mwingi ndani ya uwanja katika miaka ya karibuni, huku wachezaji wanaotoka katika taifa moja wakiweza kutiana ngumi mkononi. Marcelo anaamini Neymar atakiona cha moto.
“Ni jambo la kawaida. Tayari tumeshaonyeshana kazi na Dani Alves. Baada ya mechi tunarudi kuwa kitu kimoja tena. Itakuwa hivyo hivyo kwa Neymar. Ni rafiki yangu mkubwa, lakini hiyo haitakuwa hivyo katika mechi dhidi ya Real Madrid,” alisema Marcelo.
Marcelo alikataa kuongea lolote kuhusu uhamisho uliokwama wa staa wa Tottenham, Gareth Bale kwa madai kwamba anapenda kuwazungumzia zaidi wachezaji waliopo.

0 comments: