Instagram

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Saturday, June 15, 2013

Uganda - Tutatoza Ushuru pesa za Mobile

Uganda imetangaza kuweka kodi ya 10% kwa pesa zote zinazotumwa kwa njia ya simu na mbinu zingine za kutuma pesa.
Mganda akipiga simu
Hii itaathiri pesa zinazotumwa na Waganda waishio nchi za ng'ambo. Waziri wa fedha Maria Kiwanuka pia amesema kuwa anapanga kukusanya zaidi ya $16.5m (£10.6) kwa kutoza kodi simu zote za kimataifa kutoka nchini humo.
Bi Kiwanuka alilazimika kutafuta mbinu ya kuziba pengo la $214m katika bajeti ya serikali ya Uganda, baada ya wafadhili kupunguza msaada wao kwa Uganda kufuatia madai ya ufisadi.
Mwandishi wa BBC mjini Kampala , anasema kuwa wengi wanahofia kuwa bajeti hii, iliyosomwa Alhamisi, inawalemea zaidi watu maskini katika jamii.
Waziri Kiwanuka aliambia bunge kuwa zaidi ya $767m zilizokusanywa na serikali mwaka uliopita zilitoka kwa Waganda waishio ngambo.
Kwa mujibu wa gazeti huru nchini Uganda, Daily Monitor, ushuru huo mpya unaotozwa pesa zinazotumwa kwa simu za mkononi utaathiri zaidi ya watumiaji 8.9m wanaotumia mitandao sita ya simu nchini Uganda.

Serikali inahitaji fedha zaidi

Imeripoti pia kuwa serikali inanuia kukusanya takriban $12m kwa mwaka.
Huduma hii ya kutuma pesa kwa njia ya simu ni maarufu sana nchini Uganda ikizingatiwa kuwa raia wengi wa nchi hiyo hawana akaunti za benki.
Huhduma hii hutumiwa kuwatumia jamaa pesa nyumbani au hata kulipia madeni.

Hii bajeti sio juu ya kuweka kodi mpya, ni kukusanya tu kile ambacho hakijachukuliwa kwa muda, alisema waziri huyo.
Kwa upande wake David Holliday, mkurugenzi mtendaji wa wa shirika la mawasiliano la Telecom, kodi hii mpya bila shaka itaongeza gharama ya matumizi ya simu.
'' pesa kwenye simu imekuwa hali ya maisha ya wananchi wetu kwasababu inamaanisha kuwa hawana haja tena ya kubeba pesa taslimu.
Hata wale ambao hawakuweka pesa zao Benki sasa waliweza kuhifadhi kwenye simu zao kwasababu ni rahisi na bei nafuu'' gazeti la Daily monitor limemnukuu.

Naye Bi Kiwanuka anasema kuwa lengo la bajeti hiyo ni kuwanasa wale ambao hukwepa kulipa kodi na kuishinikiza halmashauri ya ukusanyaji ushuru kufikia malengo ya kodi ya serikali kamilifu.
Waziri wa fedha wa Uganda, Maria Kiwanuka






Wachezaji wa Super Eagles wagoma

Wachezaji wa Nigeria wameshindwa kusafiri kuelekea Brazil kufuatia mzozo kuhusu malipo ya ziada ya wachezaji.
Wachezaji wa Nigeria
Timu hiyo ya Super Eagles, inatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza siku ya Jumatatu, lakini wamesalia nchini Namibia baada ya mechi yao ya kufuzu kwa kombe la Dunia.
Wachezaji wa Nigeria, hawajafurahishwa na uamuzi wa kuwapa dola elfu mbili kila mmoja, baada ya timu hiyo kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja na Namibia mjini Windhoek.
Wachezaji hao wamesisitiza kuwa shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria ni sharfti iongeze fedha hizo maradufu kabla ya wao kusafiri.
Ripoti zinasema kuwa wachezaji hao wamesema kuwa hawawezi kusafiri kuelekea Brazil hadi mzozo huo utakapotatuliwa.
Kuna wasi wasi kuwa mabingwa hao wa Afrika huenda wakakosa kushiriki katika fainali za kombe la shirikisho, itakayo anza tarehe kumi na tano hadi tarehe thelathini mwezi huu.
Rais wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria NFF, Aminu Maigari, alifanya mazungumzo na wachezaji hao jana usiku mjini Windhoek, kuwaeleza kuwa shirikisho lake halina fedha na ndio sababu malipo hayo ya ziada yalipunguzwa.

Wiki iliyopita, vyombo vya habari nchini Nigeria, viliripoti kuwa wachezaji hao walizozana na maafisa hao wa NFF mjini Nairobi kuhusiana na malipo ya ziada baada ya Super Eagles kuilanza Harambee Stars bao moja kwa bila.
Wachezaji hao walitaka kulipwa dola elfu kumi kila mmoja kufuatia ushindi huo, lakini maafisa hao wa NFF walikataa pendekezo hilo.
NFF ambayo kwa sasa inakabiliwa na matatizo ya kifedha imelazimika kupunguza matumizi yake, likisema lilitumia kiasi kikubwa cha fedha zake katika fainali za kuwania kombe la mataifa ya Afrika iliyoandliwa nchini Afrika Kusini.
Nigeria ilikuwa imetangaza kuwa huenda ikajiondoa kwenye michuano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaoshiriki ligi ya nyumbani CHAN kutokana na matatizo ya kifedha.
Lakini uamuzi huo ulifutiliwa mbali baada ya serikali ya nchi hiyo kuingilia kati.

Wachezaji hao walitarajiwa kusafiri hadi Johannesburd leo kabla ya kuelekea nchini Brazil.


Kocha wa Nigeria








Watoto 93,000 wameuawa Syria

Umoja wa Mataifa umesema takriban watoto elfu tisini na tatu wameuawa nchini Syria tangu kuanza kwa mapigano nchini humo.
Makaburi ya watu waliouawa nchini Syria
Kwa mujibu wa takwimu hizo, idadi hiyo imeongezeka kwa zaidi ya elfu thelathini, tangu umoja huo ulipotoa takwimu zake Januari mwaka huu.
Ripoti hiyo imesema kuwa watu elfu tano hufa nchini Syria kila mwezi tangu Julai mwaka uliopita
Hata hivyo takwimu hizo huenda sio idadi kamili na Umoja wa Mataifa umesema huenda idadi ya waliouawa huenda ikawa kubwa zaidi, kwa kuwa vifo vingi havijaripotiwa.
Asilimia themanini ya waliouawa ni wanaume, lakini Umoja huo umeongeza kusema kuwa tayari umethibitisha kutokea kwa vifo vya zaidi ya watoto elfu moja mia saba ambao wako chini ya umri wa miaka kumi.
Vile vile, kuna ripoti kuwa watoto wengine waliteswa kabla ya kuuawa kinyama.
Afisa mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya haki za binadam Navi Pilllay, amesema wamepokea ripoti ya kutokea kwa mauaji ya familia nyingi wakiwa na watoto wao, ishara kuwa vita vinavyoendelea nchini Syria vimegeuka kuwa janga kuu huku maelfu ya watu wakiendelea kuuawa kila siku.
Wakati huo huo, wanaharakati wa upinzani nchini Syria na shirika la habari la serikali wamesema kuwa makombora yaliyorushwa na wanajeshi wa waasi yameanguka katika uwanja mkuu wa ndege mjini Damascus.
Moja ya makombora hayo yaliyotengenezwa nyumbani, lilianguka karibu na barabara ya kurukia ndege na hivyo kulazimisha safari kadhaa za ndege kucheleweshwa kwa sababu za kiusalama.
Shambulio hilo ndilo la kwanza katika uwanja huo wa ndege ambao kwa sasa umezingirwa na wanajeshi wa serikali.

Fastjet kutoa huduma za bei nafuu

Shirika la ndege, linalotoa huduma za usafiri wa ndege kwa bei nafuu Fastjet, limepata kibali cha kuanzisha safari za ndege za kimataifa za bei nafuu, kutoka Tanzania hadi Afrika Kusini, Zambia na Rwanda.

Ndege ya shirika la EasyJet
Kampuni hiyo inayomilikiwa na Stelios Haji-Ioannou, ambaye ni mmiliki wa shirika la ndege la Easyjet, lililo na makao yake barani ulaya.
Shirika hilo limetangaza kuwa litaanzisha safari za ndege katika mataifa hayo kwa bei nafuu huku abiria wakilipa dola mia moja pekee.
Kwa sasa shirika hilo linahudumia wasafiri nchini Tanzania pekee.
Raia wengi na hasa wafanya biashara wamefurahishwa na tangazo hilo, wakisema kuwa itapunguza gharama za usafiri na hivyo kuimarisha biashara katika kanda hiyo.
Nchini Kenya, shirika la ndege la Kenya Airways ambalo ni moja ya mashirika makubwa ya ndege barani Afrika, limepata pigo kubwa baada ya kupata hasara kubwa katika kipindi cha miaka minne iliyopita.
Ripoti zinasema kuwa shirika hilo lilipata hasara ya zaidi ya dola milioni mia moja kabla ya kutozwa ushuru, kiwango ambacho ndicho mbaya zaidi tangu mwaka wa 2009.
Shirika hilo lilikuwa maarufu sana kwa abiria wanaosafiri magharibi, mashariki, kusini na katika mataifa ya Afrika ya kati.

Afya ya Mzee Mandela imeimarika

Hali ya Afya ya aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela, inaendelea kuimarika.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, amesema kuwa amefahamishwa na madaktari wanaomtibu kuwa, hali ya Mzee Mandela ambaye anaendelea kupokea matibabu katika hospitali moja mjini Pretoria imeimarika.
Mandela amekuwa akiugua maradhi ya mapafu mara kwa mara

Rais Zuma amesema amefurahishwa na jinsi hali ya rais huyo inavyoendelea kuimarika, baada ya kudhohofika sana siku chache zilizopita.
Siku ya Jumanne rais Zuma, alisema kuwa nchi yote inazidi kumwombea Mzee Nelson Mandela ili apate afueni haraka.
Rais huyo wa zamani amelazwa hospitalini Pretoria, ambako anatibiwa maambukizi ya mapafu.
Katika taarifa yake rais Zuma amesema japokuwa Mandela ameathirika sana, madaktari wanaomshughulikia wanafanya kazi nzuri.
Rais huyo mstaafu wa Afrika Kusini, amelazwa hospitalini kwa siku ya tano leo ambako anapokea matibabu ya ugonjwa wa mapafu.
Duru kutoka kwa ofisi ya rais Jacob Zuma, zinasema kuwa Mandela mwenye umri wa miaka 94, yuko katika hali mbaya ingawa imeweza kudhibitiwa.

Familia ya Mandela

Jamaa zake pamoja na aliyekuwa mkewe Winnie Madikizela-Mandela, walimtembelea hospitalini Jumatatu
Mwanawe Mandela Zenani (Mandela-Dlamini), pia alirejea kutoka nchini Argentina, ambako yeye ni balozi.
Serikali imekuwa ikisema kuwa hali ya Mandela inatia wasiwasi ingawa madaktari wameweza kuidhibiti.
Amekuwa katika chumba ya wagonjwa mahututi tangu kulazwa hospitalini Jumamosi kwa mara ya tatu mwaka huu.
Mwezi Disemba , bwana Mandela alilazwa hospitalini kwa siku 18 baada ya kupata maradhi ya mapafu,
Kumekuwa na taarifa za simanzi kwa mara ya kwanza huku familia yake ikikusanyika kando yake, baadhi ya watu wakisema kuwa ni muda wamwache Mandela aende zake.
Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 94, alipelekwa hospitalini mapema Jumamosi , ikiwa ni mara ya tatu kulazwa hospitalini mwaka huu.
Kwa mujibu wa duru za urais, Mandela amekuwa akiugua kwa muda mjini Johannesburg baada ya kukumbwa tena na ugonjwa wa mapafu.
Msemaji wa serikali Mac Maharaj amesema kuwa maafisa katika hospitali wanataka kudhibiti idadi ya watu wanaozuru hospitali hiyo ili wampunguzie bwana Mandela usumbufu.
Alilazwa hospitalini baada ya hali yake kuwa mbaya zaidi mnamo Jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa za urais, Rais Jacob Zuma, amerejelea wito wake kwa watu nchini Afrika Kusini kumuombea Madiba wakati huu anapougua.
Lakini mwandishi wa BBC mjini Pretoria, Karen Allen, anasema kuwa kuna matumaini madogo kuwa Mandela aliyeongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, huenda akapona.
Anasema kuwa wengi walipata matumani baada ya bintiye Mandela Zindzi, kusema kuwa babake yuko salama na kuwa anaendelea kupata nafuu.
risala za heri njema na afueni kwa rais mstaafu Nelson Mandela
Mkewe Mandela Graca Machel, alifutilia mbali, ziara yake mjini London Jumamosi ili kuwa kando ya mumewe.
Mandela alikuwa Rais wa Afrika Kusini kati ya mwaka 1994 hadi 1999.
Alifungwa jela miaka 27 na anaaminika kuwahi kuugua ugonjwa wa mapafu alipokuwa akifanyishwa kazi ngumu katika machimbo ya mawe akiwa jela.

Monday, June 10, 2013

AC Milan President Adriano Galliani Adamant Stephan El Shaarawy Will Stay At San Siro

Stephan El Shaarawy
But Italians still want Tevez.
AC Milan president Adriano Galliani has insisted that young striker Stephan El Shaarawy will remain with the club next season, but still hopes that Manchester City forward Carlos Tevez will still head in the opposite direction, Sky Sports reports.
The young Italian had been linked with a switch to the Eithad this summer with the troubled Argentine heading the other way but Galliani has been quick to wave away the speculation by claiming that he still expects 20-year-old to remain at the San Siro.
Former Spurs and Portsmouth midfielder Kevin Prince Boateng has also been tipped to leave the Rossoneri this summer with Chelsea earmarked as a potential destination, however, Galliani believes that neither man will move on over the coming weeks.
“Stephan does not move from AC Milan and we have no offers for Boateng,” Galliani told Italian news source Mediaset.
But he still hopes that Manchester City striker Carlos Tevez will make the switch in the opposite direction and feels that Milan are still in pole position to land his signature despite recent links with Serie A rivals Juventus.
“Tevez is not cheating on me,” he added.
El Shaarawy has bagged 19 goals in 40 games for Milan this season and has struck up an effective partnership with another City old boy, Mario Balotelli.

(Video) Kuwait Women’s National Team Lose 21-0 to Jordan Thanks to Truly Awful Keeper


Jordan Kuwait
Shocking. Clearly the Jordan side were too strong for Kuwait in this Asian Cup qualifier but one has to wonder why they even bothered to field a keeper at all, one would imagine a cardboard cut out would fair better than the Kuwati custodian. Spotted on the always excellent 101 Great Goals.

(Video) Zinedine Zidane Shows Off His Magical Skills During Real Madrid Legends v Juventus Legends Charity Match





Zidane Legends
Still got it! Superb control by the French legend. Spotted on the always brilliant 101 Great Goals.

Saturday, June 8, 2013

Red shirt memories



Manchester United players always have one main hope when they pull on a new shirt... that it brings them further glory with the club.
Tom Cleverley and Wayne Rooney, to name just two members of the Reds' successful squad, can already point to past triumphs and the kits they associate with their personal golden moments.
For example, we asked the English pair to talk on camera about their first goals for United and discuss what they were wearing at the time. You can see the outcome in our exclusive video above.

Zaha deal delights David

Wilfried Zaha
Wilfried Zaha's arrival is not only exciting for Manchester United's future, it maintains a tradition of the present and past.
That's the view of David Gill, who signed Zaha in his last transfer deal before announcing he will step down as chief executive on 30 June. He points out the former Crystal Palace winger will increase the Reds' quota of England internationals, a core favoured by both Sir Alex Ferguson and Sir Matt Busby.
“It’s quite interesting that we recently had five players in the England team, which is good for us," says Gill, in the club's official new book Champions 20/13.
"The backbone of Manchester United has always been this way. Sir Matt Busby had it and Sir Alex [Ferguson] has nurtured it himself; this mix between British or English players and foreigners, and that’s what this club is about."
Zaha was immediately loaned back to Palace after his January sale to United was completed, enabling him to help the Eagles secure promotion back to the Barclays Premier League via last month's Championship play-off final.
“Seeing where our squad was at, it wasn’t appropriate to bring him in during January," said Gill. "It was better for him to continue playing with Palace before joining us in the summer. So we did a deal and that was a precondition, really. We were very happy when we spoke to the chairman of Palace that it was only to be done on that basis.
“He’s a player we knew and Sir Alex had been following. We’d seen him and we were
scouting him a lot in the Championship – a lot of teams were – and we just felt that because of his age, his potential and what he can bring to Manchester United it was the right thing to do – even if he’s still quite raw in a lot of respects, as a young man.
"It’s going to be a big learning curve for him [Zaha], he knows that. I think he’s going to be an exciting Manchester United player; that’s our view. He’s something different. He can beat a man, he can play in the middle or wide. It’s a great signing for us."

David Gill was speaking exclusively to Champions 20|13: How We Got The Title Back. The club's official diary of the season is on sale from 7 June.

HIZI NDIO JEZI MPYA ZA MANCHESTER UNITED MSIMU UJAO

WAYNE ROONEY






























  
TOM CLEVERLEY

Utambulisho wa Guillermo Varela ndani ya MAN UTD.

Guillermo Varela
Birthdate: 24 March 1993
Born: Montevideo, Uruguay
Position: Full-back
International: Uruguay Under-20
                                                                               





On Friday, Manchester United reached an agreement with Club Atlético Peñarol to sign Uruguayan defender Guillermo Varela.
Here, we assess the highly-rated youngster and learn more about his promising career...
The basics: Varela, who was born in Montevideo on 24 March 1993, is an ambitious full-back who plays on the right flank for South American giants Penarol in his native Uruguay.
The background: The 20-year-old has made one first-team appearance at the Centenario Stadium but is a regular for Uruguay's Under-20s with nine caps to his name.
The links: Guillermo recently completed a trial at Carrington and later spoke positively about the experience to South American radio station Tirando Paredes: “I have trained with the first-team. I am very happy and I was received very well. It was a surprise to get the chance to test myself with Manchester United. I'm glad and happy, and grateful to Penarol who allowed me to travel. I was treated so well and Chicharito helped me a lot.”
The manager: “This is what he deserves. It is a shame to see him go but you can’t deny him the opportunity to join a club like this.” – Penarol head coach Jorge Da Silva.
The future: After reaching an agreement at Carrington on Friday, Varela's next step is to fly to Turkey to represent Uruguay at the World Under-20 Championships – where future team-mates Angelo Henriquez (Chile), Sam Johnstone, Tom Thorpe and Larnell Cole (England) are also taking part. The tournament begins on Friday 21 June.
  








Friday, June 7, 2013

Usain Bolt kurejea tena baada ya jeraha


Usain Bolt mwanariadha wa Jamaica
Bingwa wa Olimpiki na mshikilizi wa rekodi ya dunia katika mbio za mita mia moja kwa wanaume Usain Bolt wa Jamaica, anatarajiwa kurejea tena uwanja baada ya kuuguza jeraha la mguu, siku ya Alhamisi wakati wa mashindano ya mbio za IAAF Diamond League mjini Rome Italia.
Bolt alipata jeraha hilo la mguu mwezi uliopita na anatarajiwa kushiriki katika mbio za mita mia moja ambapo atapamabana na mshindi wa medali ya shaba katika michezo ya Olimpiki Justin Gatlin.
Mwanariadha wa Uingereza Phillips Idowu ambaye alikosa kushiriki katika michezo ya olimpiki ya London kutokana na jeraha vile vile anarejea tena uwanjani kwa mara nyingine tena.
Idowu atapamba na bingwa wa olimpiki Christian Taylor katika mbio hizo ambazo zinatarajiwa kuwa na ushindani mkali..
Mwaka huu Bolt ameshiriki katika shindano moja pekee la mita mia moja mwezi Mei ambapo alishinda kwa ncha baada ya mshindi kuamuliwa kupitia camera za video, baada ya wanariadha wa kwanza kuonekana kumaliza kwa wakati mmoja na muda sawa wa sekunde kumi nukta sufuri tisa.

Wednesday, June 5, 2013

BREAKING NEWS! SAID LUBAWA AJIUNGA COASTAL UNIONI.

Klabu ya Coastal Union toka mjini Tanga imeendelea
 kukiboresha kikosi chake baada ya hivi punde kufanikisha
 usajili wa golikipa Said Lubawa kutoka JKT Oljoro.
Lubawa amesaini mkataba wa miaka miwili (2)
 mbele ya makamu mwenyekiti wa timu hiyo
 ndugu Steven Mguto.


 Lubuwa akisaini mkataba wa kujiunga na Coastal Union.

EXCLUSIVE: BOBAN AJIUNGA RASMI NA COASTAL UNION.

Hatimae kiungo mshambuliaji wa zamani wa Simba Haruna Moshi 'Boban' amesajiliwa rasmi na Coastal Union ya mkoani Tanga,Boban ambaye hivi karibuni alitangazwa kuachwa na klabu yake ya zamani Simba SC amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuwachezea 'wagosi wa kaya'.
Haruna Moshi aliwahi kuichezea Coastal Union mnamo mwaka 2000 ambapo alidumu hapo kwa mwaka mmoja kabla ya kujiunga na Moro UTD mnamo mwaka 2001. 
 Boban akisaini mkataba wa kujiunga na Coastal Union.
Boban akiwa ndani ya jezi ya Coastal Union akisalimiana na Kocha wa timu hiyo Hemed Moroko.

INTERVIEW YA KWANZA YA JOSE MOURINHO BAADA YA KURUDI RASMI CHELSEA




VIDEO & PHOTOS: NEYMAR ATAMBULISHWA NA KUONGEA NA MASHABIKI WA BARCELONA KWA MARA YA KWANZA @CAMP NOU




Neymar Da Silva akiingia rasmi Camp Nou baada ya kufaulu vipimo leo hii na kujiunga na Barcelona kwa mkataba wa miaka mitano.




FC Barcelona's new signing Neymar



Akisaini mkataba na Rais wa Barcelona Sandro Rosell


                                     Juggling: Neymar showed off his skills to the Nou Camp crowd

                                                                             


Tuesday, June 4, 2013

BAADA YA FIGO, ZIDANE, BECKHAM, RONALDO NA KAKA - SASA FIORENTINO PEREZ ATHIBITISHA KWAMBA MADRID INAJIANDAA KUTUMA OFA KWA SPURS KUMNUNUA BALE


REAL MADRID jana usiku imetoa tamko rasmi kwa Tottenham: Tunakuja kumnunua Gareth Bale.

Raisi Florentino Perez alikiri kwa mara ya kwanza kwamba Real Madrid wapo tayari kumsaini Bale na akitoa ishara kwamba watatuma ofa ya kwanza siku chache zijazo. 

“Inabidi tukiboreshe kikosi chetu tena kwa umakini mkubwa - hilo litafanyika ndani wiki chache zijazo.” 
Perez pia alikiri kwamba ameshakutana mwenyekiti wa Spurs Daniel Levy mwaka jana kuzungumzia juu ya usajili wa Bale.

Aliongeza: "Bale ni mmoja ya wachezaji wakubwa barani ulaya na Real Madrid siku zote timu yetu imekuwa na wachezaji wakubwa wa soka.
"Nilikutana na mwenyekiti wa Tottenham mwaka jana na haki na majukumu ya kutetea maslahi ya timu yake. 
"Kuhusu bei iliyozungumziwa kuhusu Bale, wachezaji hawana bei kubwa au ndogo - wao ni kama uwekezaji kwenye biashara ya soka. 
"Wachezaji wenye gharama zaidi  ni wale ambao mara zote huwa ni uwekezaji kwenye biashara, na ikiwa watacheza vizuri basi lzima watengeneze faida kwenye uwekezaji huo." 

Maneno ya Perez yanabeba uzito mkubwa ukizingatia ndio mtu aliyefanikisha dili kubwa kabisa kwenye historia ya soka duniani za usajili wa Luis Figo, Zinedine Zidane, David Beckham, Kaka na Cristiano Ronaldo.

Simba yajiondoa mashindano ya CECAFA

Klabu ya Simba kutoka Tanzania, imetangaza kuwa haitashiriki katika michuano ya kuwania kombe la klabu bingwa kanda ya Afrika Mashariki na Kati CECAFA, ikiwa itaandaliwa katika jimbo la Darfur nchini Sudan.
Nicholas Musonye katibu mkuu wa CECAFA
Uamuzi huo umechukuliwa kufuatia mjadala ulioibuka katika bunge la Tanzania baada ya waziri wa mambo ya nje wa Tanzania Benard Membe kuhoji hali ya Usalama katika eneo hilo.
Mwenyekiti wa klabu ya Simba, Ismail Adne Rage, amesema uongozi wa CECAFA ni sharti ubadilishe mahala pa fainali hizo la sivyo wao hawatashiriki.
''Hatuwezi kwenda Darfu kuvalia mavazi yasiyopenya risasi'' Alisema Bwana Rage.
''Ni wazi kuwa hali ya usalama katika eneo hilo sio nzuri kama ilivyothibitishwa na serikali'' Aliongeza mwenyekiti huyo wa Simba.
Membe aliliambia bunge la Tanzania kuwa alishangazwa sana na uamuzi wa kuandaa fainali hizo katika eneo la Darfur ambalo limekubwa na mapigano ya mara kwa mara.
Membe amesema serikali ya Tanzania, inachunguza hali ilivyo na kuwa watachukua uamuzi muafaka kuhusiana na suala hilo.
''Hatuwezi kuwatuma vijana wetu katika eneo ambalo hatuna hakikisho la Usalama'' Alisema Membe.
Mabingwa watetezi Yanga, vile vile kutoka Tanzania ambao walikuwa wameonyesha nia ya kushiriki katika fainali hizo za Darfur, pia nao wanasema watafuata ushauri kutoka kwa serikali.
Katibu mkuu wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Tanzania TFF, Generali Anfetile Osiah, amesema wao wamehakikishiwa usalama na eneo watakalopiga kambi wakati wa mashindano hayo.
Endapo timu hizo mbili kutoka Tanzania zitajiondoa kutoka kwa fainali hizo, itakuwa pigo kubwa kwa waandalizi wa mashindano hayo.
Timu mbili kubwa nchini Sudan Al Hilal na Al Merreikh tayari zimethibitisha kuwa hazitashiriki kutokana na hofu sa kiusalama.
Katibu mkuu wa CECAFA, Nicholas Musonye amekariri kuwa eneo hilo la Darfur ni salama kuwa mwenyeji wa mashindano hayo.

Mourinho ateuliwa kocha mpya wa Chelsea


Klabu ya Chelsea imethibitisha kuwa Jose Mourinho ametueliwa rasmi kuwa kocha mpya wa klabu hiyo.           Mourinho amesaini mkataba wa miaka minne na anarejea tena Chelsea ambako aliisaidia kushinda kombe la ligi kuu ya premier mara mbili, kombe la FA na mawili ya kombe la ligi kati ya mwaka wa 2007 na 2007. Afisa mkuu mtendaji wa klabu ya Chelsea, Ron Gournlay, amesema '' Bodi ya wakurugenzi ya Chelsea ina fahari kutangaza rasmi kuwa Jose Mourinho ametuliwa kuwa kocha mpya na ni fahari yai kumkaribisha tena katika klabu hiyo''.

Gournlay aliendelea kusema kuwa, mafanikio yake na nia yake ya kuandikisha matokeo mema zaidi yalimfanya kuwa mgombea anayestahili kupewa nafasai hiyo.
'' Ni nia yetu kusonga mbele na kuifanya klabu yetu ipate matokeo mema zaidi na chini ya uongozi wa Mourinho, naamini kuwa Chelsea itapata mafanikio zaidi kwa kuwa yeye ndiye chaguo letu nambari moja'' Alisema afisa huyo.
Mourinho alikuwa na ufuasi na ushawishi mkubwa wakati na hata baada ya kukihama klabu ya Chelsea.

Wasifu wa Mourinho



Tangu alipokihama klabu ya Chelsea mwaka wa 2007, Mourinho alifanya kazi nchini Italia na klabu ya Inter Milan, kabla ya kujiunga na klabu ya Real Madrid ya Uhispania ambako alishinda vikombe vitatu vya ligi kuu, mawili ya ligi shirikisho na kombe la klabu bingwa barani Ulaya.
Mourinho akiwa na Real Madrid
Mourinho aliteuliwa kuwa kocha wa Chelsea mara ya kwanza mwaka wa 2004, miezi michache baada ya kushinda kombe la klabu bingwa barani ulaya na klabu ya FC Porto, na February mwaka wa 2005 alishinda kombe lake la kwanza wakati Chelsea ilipoishinda Liverpool kwa magoli matatu kwa mawili katika fainali ya kombe la Carling.
Mwaka huo Chelsea ilishinda ligi kuu ya Premier kwa kuzoa jumla ya alama tisini na tano na kufungwa magoli 15 tu katika mechi Thelathini na nane.
Msimu wa mwaka wa 2005-2006 Chelsea ilishinda tena kombe la ligi kuu kwa taadhima kuu pale ilipoinyuka Machester United magoli matatu kwa bila.
Baada ya hapo Chelsea iliishinda Arsenal katika fainali ya kombe la Carling mjini Cardiff na pia kombe la FA wakati Manchester United haikuwa imepoteza mechi yoyote katika uwanja mpya wa Wembley.
Mwaka wa 2007, Mourinho alijiuzulu baada ya kushauriana na wasimamizi wa Chelsea na kujiunga na klabu ya Inter Milan ya Italia.


Akiwa na Inter Milan alishinda mataji mawili ya ligi ya Seria A na kombe la klabu bingwa Marani Ulaya.
Mourinho akiwa na Frank Lampard

Kocha huyo kisha alijiunga na Real Madrid ambako alishinda kombe la La Liga na lile la Copa Del Rey na kumaliza majukumu yake kama kocha nchini Uhispania hiyo jana.
Mourinho anarejea Chelsea na baadhi ya maafisa wake wa kiufundi Rui Faria, Silvio Louro na Jose Morais.
Kila mmoja wao atakuwa na jukumu na cheo cha naibu kocha mkuu na watashirikiana na maafisa wanaohudumu na Chelsea kwa sasa ikiwa ni pamoja na Steve Holand, Christophe Lollichon na Chris Jones.

Mourinho atajulishwa rasmi kwa wachezaji na mashabiki wa klabu hiyo tarehe kumi mwezi huu katika uwanja wa Stamford Bridge.

Saturday, June 1, 2013

OFFICIAL: RADAMEL FALCAO MCHEZAJI MPYA WA MONACO



Hatimaye mshambuliaji nyota wa klabu ya Atletical de madrid ya Hispania RADAMEL FALCAO ametia saina ya kuitumikia timu ya AS MONACO inayoshiriki katika LIGEUE 1 ya nchini Ufaransa.

TAIFA STARS WATAKIWA KUJITUMA KUHAKIKISHIA WANARUDI NA USHINDI NA KUFUZU KOMBE LA DUNIA


Balozi wa Tanzania nchini Ethiopia, Joram Biswaro amewataka wachezaji wa Taifa Stars kuhakikisha wanaipeleka timu hiyo kwenye fainali za Kombe la Dunia zitakazofanyika mwakani nchini Brazil.

Ametoa changamoto hiyo wakati alipotembelea mazoezi ya timu hiyo jana (Mei 29 mwaka huu).

Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imepiga kambi nchini Ethiopia na inafanya mazoezi kwenye Uwanja wa Addis Ababa.

“Watanzania tunafurahi kutokana na uwezo mnaouonyesha, hasa baada ya kuifunga Morocco mabao 3-1. Kama mliwafunga nyumbani hata kwao mnaweza kuwafunga. Tunataka kuwaona Maracana (Brazil) mwakani, mimi tayari ninayo tiketi mtanikuta kule,” amesema Balozi Biswaro ambaye enzi zake aliwahi kuichezea timu ya Yanga.

Taifa Stars ambayo iko Addis Ababa tangu Jumatatu (Mei 27 mwaka huu) imeweka kambi katika hoteli ya Hilton ambapo Jumapili (Juni 2 mwaka huu) itacheza mechi ya kirafiki na Sudan (Nile Crocodile) kwenye Uwanja wa Addis Ababa.

Balozi Biswaro ameikaribisha Taifa Stars ubalozini Addis Ababa mara baada ya mechi dhidi ya Sudan ambapo itakutana na baadhi ya Watanzania wanaoishi Ethiopia kabla ya kuondoka alfajiri kwenda Marrakech, Morocco kwa kupitia Cairo, Misri.

Kocha Kim Poulsen amesema kikosi chake kinaendelea na mazoezi vizuri na kitaimarika zaidi baada ya wachezaji Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanaochezea timu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC) kujiunga nacho Juni 3 mwaka huu jijini Marrakech kwa ajili ya mechi dhidi ya Morocco itakayochezwa Juni 8 mwaka huu.

Naye Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe, akizungumza kutoka Dar es Salaam, alisema wao kama wadhamini wamefarajika kuona timu inaendelea vizuri Mjini Addis na  inaleta matumaini kuwa watacheza vizuri katika mechi dhidi ya Morocco Juni 8.
 “Tuna imani sana na Taifa Stars kwani wameshatuonesha yote yanawezekana…watanzania waiombee timu yetu ili na sisi tupate nafasi ya kucheza Brazil mwakani,” alisema.


Wachezaji walioko katika kikosi cha Stars jijini Addis Ababa ni Juma Kaseja, Aggrey Morris, Mwadini Ally, Ally Mustafa, Shomari Kapombe, Kevin Yondani, Erasto Nyoni, Haroub Nadir, Mwinyi Kazimoto, Frank Domayo, Mrisho Ngasa, Khamis Mchana, Amri Kiemba, Salum Abubakar, Simon Msuva, John Bocco, Vicent Barnabas, Mudathiri Yahya, Athuman Idd, Haruni Chanongo na Zahoro Pazi.

Daily Monitor hatimaye lafunguliwa

Gazeti la Daily Monitor nchini Uganda, limefungua ofisi zake leo baada ya kufungwa na maafisa wa polisi kwa zaidi ya wiki moja.
Gazeti hilo la binafsi, lilifungwa baada ya kuchapisha barua inayodai kuwa rais Yoweri Museveni anamuandaa mwanawe kumrithi kama rais .
Barua hiyo inayosemekana kutoka kwa generali wa jeshi, ilisema kuwa wale waliokuwa wanapinga mpango wa Museveni , huenda wakauliwa.
Taarifa ya serikali ilisema kuwa wamiliki wa gazeti hilo, wameelezea kusikitishwa kwa kuchapishwa kwa taarifa hiyo.
Setesheni mbili za redio zilizo chini ya kampuni ya Daily Monitor pia zilifungwa .
Wafanyakazi wa gazeti hilo walisema kuwa polisi waliokuwa wamezingira ofisi za kampuni hiyo kwa siku kumi na moja zilizopita, wameanza kuondoka katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa taarifa ya gazeti hilo kwenye mtandao wafanyakazi wa gazeti hilo, wameweza kurejea kazini huku polisi wakionekana kuzifungua ofisi hizo.
Gazeti la Red Pepper pia lilifungwa kwa kuripoti madai hayo.
Museveni amekuwa mamlakani tangu mwaka 1986 na uchaguzi unatarajiwa kufanyika mwaka 2016.
Kumekuwa na tetesi kuwa mwanawe Museveni, Bregedia Muhoozi Kainerugaba, anaandaliwa kuweza kumrithi Museveni atakapoondoka mamlakani .
Hata hvyo serikali imekanusha madai hayo na kusema kuwa haina mpango wowote kama huo.

Msako kuendelea

Mapema wiki hii, polisi walitumia gesi ya kutoa machozi pamoja na virungu wakati wakiandamana nje ya ofisi za gazeti hilo.
Maafisa wa utawala wanasema kuwa walitaka ushahidi kuhusu namna gazeti la Daily Monitor lilivyopata barua hiyo ya siri , inayodaiwa kuandikwa na Generali David Sejusa, ambaye yuko nje ya nchi.
Kwenye taarifa ya serikali, msako uliofanywa tarehe 20 mwezi Mei mwaka 2013 uliamrishwa kwa sababu ilisemekana kuwa katibu mkuu wa usalama wa ndani, ambaye barua hiyo ilikuwa inatumwa kwake pamoja na maafisa wengine walionuiwa kupokea barua hiyo ambayo hata hiuvyo hawakuweza kuipokea. Baadaye ilijulikana kuwa ni kampuni ya Daily Monitor pekee iliyokuwa na barua hiyo
Rais Museveni na wakuu wa kampuni ya vyombo vya habari ya Nation , inayomiliki Monitor, walikutana siku ya Jumapili kujadili hali ya gazeti la Daily Monitor.
Walikubaliana kuwa wachapishe taarifa walizo na uhakika nazo na ambazo vyanzo vyake vinaweza kuaminika.
Pia walikubaliana kuwa maakini na taarifa ambazo zinaweza kusababisha hali ya taharuki , chuki za kikabila na kusababisha utovu wa usalama.

Wabunge wa Kenya wapata pigo


Maandamano Mali dhidi ya Ufaransa

Wapiganaji wa Tuareg wanaodhibiti mji wa Kidal
Maelfu ya watu mjini Gao Kaskazini mwa Mali, wamefanya maandamano wakituhumu Ufaransa kwa kupendelea mahasimu wao wa kabila laTuareg.
Waandamanaji walisema kuwa Ufaransa ina mapendeleo katika kile kinachoonekana kama kabila la Tuareg kuendelea kudhibiti mji wa Kidal
Tuuareg wanaotaka kujitenga wanasema kuwa hawatawaruhsu maafisa wa utawala nchini Mali kuingia Kidal huku uchaguzi ukiandaliwa kufanyika mwezi Julai.
Ufaransa, iliongoza operesheni ya kijeshi kuwafursha waasi waliokuwa wameteka sehemu ya Kaskazini mwa nchi mapema mwaka huu.
Aidha wanajeshi wa Ufaransa walianza kuondoa baadhi ya wanajeshi wake 4,000 kutoka nchini humo mwezi Aprili na inapanga kuikabidhi jukumu la ulinzi wanajeshi wa nchi hiyo
Waandalizi wa maandamano yaliyofanyika hapo jana walisema kuwa takriban waandamanaji 3,000 walishiriki kwenye maandamano hayo, ingawa maafisa walisema kuwa idadi yao ilikuwa ndogo.
Maandamano hayo yaliandaliwa na makundi ya kiraia yenye kutoa ulinzii kwa raia walioelezea ghadhabu yao kwa kutohusishwa katika mazungumzo ya kuleta amani Kaskazini mwa nchi.
Makundi hayo, yalisema kuwa kundi la Tuareg, lilialikwa kwenye mazungumzo, ya amani nchini Burkina Faso bila wao kushirikishwa.
"tunataka Ufaransa ituambie wanachonuia," alisema mwanadamanaji Moussa Boureima Yoro aliyenukuliwa na shirika la habari la AFP
"wanatuchanganya wanaposema kwa upande mmoja kuwa Kidal ni sehemu ya Mali wakati huku kwingine wakijifanya kama sivyo kwa kuepndelea Tuareg.''
Hamil Toure, mmoja wa waandamanaji alimbia BBC kuwa makundi ya vijana yangali yamejihami na kuwa yatazuia uchaguzi kufanyika ikiwa mahitaji yao hayatatimizwa.
Wananchi wengi wa Gao wanalaumu kabila la Tuareg, kwa kuwa chanzo cha mapigano nchini Mali.

Vijana wa Malawi waenda Korea kwa ajira

Rais Joyce Banda anasema Malawi inakabiliwa na wakati mgumu kuhusu ajira kwa vijana
Serikali ya Malawi, imetetea mpango wake tatanishi ulioafikiwa na Korea Kusini kusafirisha hadi vijana wake laki moja kufanya kazi kama wafanyakazi wahamiaji.
Wabunge wa upinzani wametaja mpango huo kama biashara ya utumwa.
Lakini waziri wa wafanyakzi nchini humo anayekabiliwa na wakati mgumu kuwatafutia ajira vijana amekanusha madai hayo.
Eunice Makangala, aliambia BBC kuwa alitaka tu kusaidia vijana wa Malawi wanaotarajiwa kwenda Seoul kutafutiwa ajira.
Mwandishi wa BBC mjini Blantyre anasema, Rais Joyce Banda, aliweka mkataba huo na serikali ya Korea Kusini wakati alipozuru nchi hiyo mwezi Februari, mwaka huu.
Makubaliano hayo yatashuhudia vijana wenye kati ya umri wa miaka 18-25 kupata kazi katika viwanda vya nchi hiyo na hata kwenye mashamba katika rasi ya Korea.
Hakuna takwimu rasmi za viwango vya ukosefu wa ajira nchini Malawi, kwa sababu ya kutokuwepo mfumo wa kutambulisha watu, kuweza kujua idadi ya wasio na ajira.
Lakini utafiti wa hivi karibuni unaonyesha kuwa 80% ya wanafunzi wanaomaliza vyuo vikuu hurejea vijijini kila mwaka kwani hawezi kupata kazi mijini.
Lakini wabunge wa upinzani wameghadhabishwa mno kwa sababu ya mpango wa kutaka kuwasfirisha vijana hao kutafuta kazi nchini Korea.
''Daima sisi hulalamika kuhusu wataalamu wetu kwenda kutafuta ajira katika nchi za kigeni, na hata kuwashawishi raia wa Malawi wanaoishi katika nchi za kigeni kurejea nyumbani, wakati hapa tunawapeleka vijana kutafuta ajira nje? alilalamika mbunge mmoja.
Bi Makangala aliambia BBC kuwa wameafikia mpango huu kwa nia njema.
''Sio utumwa mambo leo'', alisisitiza bi Makangala
''Kuna watu wanaofanya hapa kazi na ambao wanatoka Misri, Nigeria, India na Uingereza.''
"je unataka kuniambia watu hao ni watumwa? Na viwango vya ukosefu wa ajira viko juu sana .''
Lakini Henry Kachaje,ambaye ni mtaalamu wa maswala ya ajira alisema kuwa mktaba ungeweza kuafikiwa vyema kuliko makubaliano ya sasa. Kuwa serikali ingwavutia wakeezaji kuja nchini humo na kutoa nafasi ya ajira kwa vijana.