Instagram

This is default featured slide 3 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 4 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

This is default featured slide 5 title

Go to Blogger edit html and find these sentences.Now replace these sentences with your own descriptions.This theme is Bloggerized by Lasantha Bandara - Premiumbloggertemplates.com.

Thursday, December 12, 2013

Mandela aivuta dunia kuhamia Afrika Kusini


Mashada na Picha ya Rais mstaafu wa Afrika Kusini Marehemu Nelson Mandela anayetarajiwa kuzikwa jumapili ya tarehe 15 Disemba, 2013  


Johannesburg. Viongozi zaidi ya sabini wakiwamo wakuu wa nchi na Serikali wanatarajiwa kushiriki hatua mbalimbali za safari ya mwisho ya Mzee Mandela aliyefariki Alhamisi ya Desemba tano usiku.
Anatarajiwa kuzikwa Jumapili ijayo, Desemba 15, 2013 katika Kijiji cha Qunu alikokulia, mazishi ambayo yanatarajiwa kuwavuta maelfu ya watu kutoka kona mbalimbali za dunia.
Hata hivyo hadi jana maofisa wa Serikali ya Afrika Kusini walisema walikuwa bado hawajapata orodha kamili ya viongozi wote watakaohudhuria, l pia wakashindwa kusema iwapo Rais Obama atakwenda Qunu au atashiriki katika hatua nyingine za awali za msiba huo kabla ya mazishi ya Jumapili.
Msemaji wa Ikulu ya Marekani, Jay Carney alinukuliwa akithibitisha kwamba Obama na mkewe Michele watashiriki katika msiba huo lakini hakuwa tayari kueleza suala hilo kwa undani. Habari zaidi zilizopatikana jana mjini Johanesburg zinasema Rais wa Brazil, Dilma Rousseff atakuwa miongoni mwa wageni mashuhuri watakaoshiriki.
Balozi wa Marekani nchini Afrika Kusini, anasema kuwa: “Rais Obama, amethibitisha kushiriki mazishi ya Madiba” (akirejea) jina maarufu la Mzee Mandela, taarifa ambayo ilitiliwa na nguvu na habari zilizoinukuu Ikulu ya Washington ikithibitisha ujio wa kiongozi huyo pamoja na watanguliza wake; George W. Bush na Bill Clinton.
Vyombo mbalimbali vya habari vilinukuu taarifa ya Ikulu ya Marekani ikisema: “Rais Obama na mkewe watakwenda Afrika Kusini wiki ijayo kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa ajili ya kumbukumbu ya Nelson Mandela na watashiriki katika tukio hilo la kukumbukwa.”
Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma alitangaza ratiba ya maombolezo ya shujaa huyo aliyeongoza vita dhidi ya sera za ubaguzi wa rangi zilizokuwa zikitekelezwa na Makaburu na jana ilikuwa ni siku ya maombi ya kitaifa kwa ajili ya Mzee Mandela.
Leo Jumanne kutakuwa na tukio la kitaifa katika Uwanja wa Michezo wa FNB, Johannesburg ambako ni sehemu ya hitimisho ya safari ya Mandela huku watu zaidi ya 80,000 wakitarajiwa kuhudhuria na kati ya kesho Jumatano na Ijumaa, mwili wa Mandela utakuwa katika Majengo la Umoja (Union Buildings) Pretoria ambako utaangwa kwa siku tatu mfululizo.
Mkurugenzi wa Habari na Mawasiliano wa Afrika KusiniNeo Momodu aliwaambia waandishi wa habari jijini Johannesburg kuwa watuwa Pretoria watakuwa na nafasi ya kushuhudia mwili wa Mandela ukisafirishwa kutoka chumba cha kuhifadhia maiti kwenda Jengo la Umoja kila asubuhi kwa siku tatu mfululizo.
Momudu anasema mitaa ambayo mwili huo utakuwa ukipitishwa itatangazwa ili kuwezesha wakazi wake na wananchi wengine kupata fursa ya kujipanga pembezoni mwake kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho kwa kiongozi huyo.
“Njia ambazo mwili wa marehemu utakuwa ukipitishwa kila asubuhi kutoka chumba cha kuhifadhia kwa ajili ya kupelekwa kupewa heshima za mwisho, zitatangazwa na tutawaomba wananchi kujipanga pembezoni mwa njia hizo wakati mwili huo ukipita katika mitaa hiyo ya Pretoria,” anasema.
Hata hivyo, Momodu anasema utaratibu wa kutoa heshima za mwisho utaratibiwa na kuna uwezekano mkubwa kwamba si kila mtu atakayeweza kuingia katika eneo hilo na kwamba kila mmoja atakayeingia lazima awe na kitambulisho maalumu.
 Anasema kutakuwa na eneo maalumu la kusubiri kuingia kwa ajili ya kutoa heshima za mwisho na kwamba watakafanikiwa kupata ruhusa ya kwenda kuaga, watakuwa wakipakiwa kwenye mabasi maalumu yaliyoandaliwa kwa ajili ya kazi hiyo na watarejeshwa na mabasi hayo.
Jumamosi, Desemba 14, mwili wa Mandela utasafirishwa kwenda Qunu ambako Jumapili Desemba 15, utazikwa rasmi.

Friday, August 30, 2013

LEO NDIO LEO CHEKA VS WILLIAMS.

b
Bondia Francis Cheka (kushoto) na Phil Williams kutoka Marekani, kwa pamoja wakiwa wameshika Taji la Ndondi la Dunia (WBF) mara baada ya kumaliza kupima uzito katika  Ukumbi wa Idara Habari Maelezo jana, tayari kuzikunja leo kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam. Picha na Michael Matemanga. 
Dar es Salaam. Bingwa wa Masumbwi, Francis Cheka amesema dhamira ya kumtandika mpinzani wake, Phil Williams kutoka Marekani katika pambano lao usiku wa leo, iko palepale.
“Siwezi kumwangusha Rais Jakaya Kikwete, namwahidi nitashinda mchezo wa leo na kuubakisha mkanda wa ubingwa Tanzania,” alisema Cheka wakati akiongea na Mwananchi jana.
Cheka anashuka ulingoni, Diamond Jubilee kuzikunja na Williams katika pambano la kuwania Ubingwa wa Dunia (WBF), huku Makamu wa Rais, Gharib Bilal akiwa mgeni rasmi kumwakilisha Kikwete.
Mabondia hao, jana walipima uzito jijini Dar es Salaam tayari kwa pambano hilo linalosubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa ndondi nchini.
“Najua JK (Jakaya Kikwete) ni mpenda michezo na anatoa sapoti kwenye michezo, hivyo namwahidi kufanya kweli leo,” alisema Cheka na kuongeza: “Nimejipanga kushinda pambano hili, nilishasema tangu awali, narudia kusema tena, sitawaangusha mashabiki wangu.”
Aliongeza: “Niko tayari kufia uwanjani, lakini siyo kuliona taji linaondoka Tanzania. Nitamaliza kazi kwa mafanikio.
Kwa upande wake, Williams alisema amekuja kushindana na siyo kinyume chake, hivyo anajiandaa kutoa upinzan mkali dhidi ya mpinzani wake.
Mwanamasumbwi huyo anashuka dimbani ikiwa ni wiki mbili kupita tangu amshinde kwa pointi bondia wa Malawi, Chiotcha Chimwemwe. Pia kutakuwa na mapambano ya utangulizi kati ya Thomas Mashali na Mada Maugo watakaowania Ubingwa wa WBF Afrika.

Eto'o asaini mkataba na Chelsea

Samuel Eto'o
Chelsea imemsajili mshambuliaji wa Cameroon, Samuel Eto'o kutoka klabu ya Anzi Makhachkala ya Urussi.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka thelathini na miwili amesaini mkataba wa mwaka mmoja na Chelsea.
Kocha wa Chelsea Jose Mourinho, aliamua kumsajili Eto'o baada ya maombi yake ya kumsajili nyota wa Manchester United Wayne Rooney kukataliwa.
Mapema wiki hii, ilibainika kuwa Rooney hakuwa tayari kulazimisha uhamisho wake kwa kuwasilisha ombi lake la kutaka kuondoka na hivyo kuzima matumaini ya Chelsea ya Kumsajili mchezaji huyo.
Mchezaji huyo ambaye ni mshindi mara nne wa mchezaji bora wa soka barani Afrika, alikuwa nyota wa AC Milan mwaka wa 2010 wakati Mourinho alipoiongoza kushinda kombe la klabu bingwa barani Ulaya.
Mwaka wa 2011, Eto'o alivunja rekodi ya kuwa mchezaji anayelipwa mshahara mkubwa zaidi duniani.
Klabu hiyo ya Anzi pia imemuuza kiungo wake Willian, mwenye umri wa miaka 25 kwa klabu ya Chelsea, baada ya mmiliki wa klabu hiyo mfanya biashara tajii Suleyman Kerimov kupunguza bajeti ya klabu hiyo.
Samuel Eto'o katika kikao na waandishi wa habari
Eto'o alianza kucheza soka ya kulipwa na klabu ya Real Madrid, lakini alisajiliwa na vilabu vya Leganes na Real Mollorca kwa mkopo kabla ya kupata mkataba wa kudumu Mallorca mwaka wa tisini na tisa.
Mchezaji huyo ambaye alikuwa katika kikosi cha Cameroon kilichoshinda kombe la mataifa ya Afrika mwaka wa 2002, vile vile alishinda kombe la Copa del Rey, kabla ya kujiunga na klabu ya Barcelona mwaka wa 2004.
Akiwa katika uwanja wa Nou Camp, alishinda kombe la klabu bingwa barani ulaya mara mbili mwaka wa 2006 na 2009 na alifunga bao katika fainali hizo mbili pamoja na kushinda kombe la ligi kuu ya La Liga mara tatu.
Mwaka wa 20098, Barcelona iliilipa Inter Milan pauni milioni arubaini pamoja na mchezaji huyo ili kumsajili Zlatan Ibrahimovic na mshambuliaji huyo alifanikiwa kushinda kombe la klabu bingwa barani Ulaya kwa mara nyingine chini ya Uongozi wa Mourinho katika uwanja wa San Siro.
Alijiunga na klabu ya Anzi na ripoti zinasema kuwa alikuwa akilipwa £167,825 kwa wiki mwaka wa 2011

Wednesday, August 28, 2013

ROBERT WAPOTEEN PHOTO ALBUM


ROBERT WAPOTEEN & BAKARI MTEKUFA


TEAM KILA KITU

TEAM WAKALI WA MEDIA

TEAM RESEACHER


Posted by Picasa

Miaka 50 ya "I have a dream"

Martin Luther King

Imetimia miaka 50 tangu Martin Luther King alipotoa hotuba yake ya kihistoria. King aliyekuwa mwanaharakati wa kupigania haki za watu weusi Marekani, alizungumzia ndoto yake ya kuwa na nchi yenye usawa kwa wote.
"Nina ndoto kwamba siku moja watoto wangu wanne wataishi kwenye nchi ambapo hawatatathminiwa kulingana na rangi ya ngozi yao bali kulingana na tabia yao." Ilikuwa tarehe 28 Agosti mwaka 1963, pale ambapo Martin Luther King na maelfu ya Wamarekani weusi waliandamana mjini Washington kudai uhuru na haki sawa ya kupata ajira kwa watu weusi. King alikuwa miongoni mwa waandalizi wa maandamano hayo na mmoja wa watu waliotoa hutoba siku hiyo. Hotuba yake ya I have a dream - yaani nina ndoto - inaelezea mustakabali anaoutamani kwa nchi yake. Alitaka Marekani iwe na umoja na watu wasibaguliwe kwa sababu ya rangi ya ngozi yao.
"Hatuwezi kuridhika iwapo mtu mweusi kutoka Mississippi hana haki ya kupiga kura na mtu mweusi anayeishi New York haoni sababu ya kupiga kura," alisema King katika hotuba yake. Miaka hamsini baadaye, sehemu fulani ya ndoto ya Martin Luther King imetimia. Kwa mara ya kwanza Marekani inaongozwa na rais mweusi.
Ubaguzi bado tatizo sugu
Barack Obama ni rais wa kwanza mweusi wa MarekaniBarack Obama ni rais wa kwanza mweusi wa Marekani
Barack Obama leo ataongoza maadhimisho ya miaka 50 ya hotuba ya King. Atatoa hotuba kwenye jengo la kumbukumbu ya Lincoln mjini Washington - mahali pale pale ambapo King alielezea ndoto yake miaka 50 iliyopita.
Obama ameeleza kuwa mafanikio yake kama mwanasiasa mwenye mamlaka makubwa zaidi Marekani, yamejengwa juu ya misingi ya juhudi za Martin Luther King na wenzake. Anaamini kwamba asingekuwa rais wa Marekani leo, kama wanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi wasingekuwa tayari kuvumilia vitisho, mateso na hata kufungwa jela.
Hata hivyo, ubaguzi wa rangi bado ni tatizo sugu kwenye baadhi ya maeneo ya Marekani. Kisa cha kijana Trayvon Martin aliyepigwa risasi na Mmarekani mwenye ngozi nyeupe aliyehisi kuwa Treyvon ni kibaka kiliweka wazi kwamba bado yapo maoni potofu juu ya watu weusi. Suala lililozusha mjadala mkubwa zaidi ni kwamba aliyempiga risasi kijana huyo hakupewa hukumu yoyote mahakamani.
Sherehe za leo za mjini Washington zitahudhuriwa pia na marais wa zamani wa Marekani. Bill Clinton na Jimmy Carter ni miongoni mwa wale watakaotoa hotuba.

DOWNLOAD NEW SONG - Shebby Love ft Mabeste-Mapenzi Basi



Zimbabwe kujenga bustani ya kifahari

Bwawa la Victoria



Serikali ya Zimbabwe imetangaza mpango wa kujenga kivutio cha kitalii, "Disneyland in Africa" katika maporomoko ya maji ya Victoria ili kuimarisha secta ya utalii nchini humo.
Waziri wa utalii wa Zimbabwe Walter Mzembi ameiambia BBC kuwa serikali ya nchi hiyo itatumia dola milioni mia tatu kujenga bustani hiyo.
Serikali ya nchi hiyo inajaribu kufufua secta ya utalii iliyosambaratika kufuatia mzozo wa kisiasa uliodumu kwa takriban miaka kumi iliyopita na kushuka kwa dhamani ya safaru ya nchi hiyo.
Rais Robert Mugabe alichaguliwa kuhudumu kuwa rais wa nchi hiyo kwa muhula wa saba katika uchaguzi mkuu uliokamilika mwezi uliopita.
Lakini waziri huyo amesema, serikali yake haitategemea maporomoko hayo ya maji ya Victoria pekee, lakini amesema bwawa hilo linauwezo wa kuinua uchumi wa taifa hilo kwa kiasi kikubwa.
''Tunafikiria kuijenga bustani hiyo ili iwe sawa na bustani ya Disneyland nchini Marekani, na itajumuisha hoteli za kifahari, medani ya burudani, hoteli na vifaa vya kuandaa mikutano. Hii ndio maoni yetu na tunahitaji watu ambao wataweza kuiendesha'' Alisema waziri huyo.
Awali Mzembi aliliambia shirika la habari la serikali la nchi hiyo kwua serikali ya rais Robert Mugabe inadhamiria kuanzisha mfumo ambao utaruhusu soko huria katika secta ya mabenki nchini humo, ambapo watu ambao sio raia wa nchi hiyo wanaweza kufungua akaunti nchini humo.
Waziri huyo aliyasema hayo wakati wa mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu utalii unaoandaliwa kwa pamoja na Zimbabwe na Zambia.
Uamuzi huo wa kuipa Zimbabwe fursa ya kuandaa kongamano hilo la Umoja wa Mataifa, umeshutumiwa vikali na shirika la kutetea haki za kibinadam la Umoja huo, lililo na makao yake mjini Geneva, likadai serikali ya nchi hiyo inaendelea kukiuka haki za kibinadam na kuwa uchaguzi uliokamilika hivi majuzi haukuwa huru na wa haki.
Serikali ya Zimbabwe pia inapanga kupanua uwanja wa Ndege wa Victoria Fall, mradi ambao utagharimu dola milioni mia moja hamsini.
Katika kipindi cha miezi mitatu ya kwanza mwaka huu, secta ya utalii nchini humo ilikuwa kwa asilimia kumi na saba na ikiwa uthabiti wa taifa hilo utadumishwa secta ya utalii ina uwezo wa kuchangia pato la taifa hilo kwa asilimia kumi na tano.

DOWNLOAD NEW HIT AMINI FT BARNABA-WHY MIMI.







Wednesday, August 21, 2013

Marcelo ampania Neymar El Classico!


           


MADRID, HISPANIA
INGAWA wanacheza pamoja katika timu ya taifa ya Brazil, lakini beki wa kushoto wa Real Madrid, Marcelo amempania vilivyo staa mpya wa Barcelona, Neymar, wakikutana katika mechi ya El Classico.
Mechi hiyo imekuwa ikizua ukorofi mwingi ndani ya uwanja katika miaka ya karibuni, huku wachezaji wanaotoka katika taifa moja wakiweza kutiana ngumi mkononi. Marcelo anaamini Neymar atakiona cha moto.
“Ni jambo la kawaida. Tayari tumeshaonyeshana kazi na Dani Alves. Baada ya mechi tunarudi kuwa kitu kimoja tena. Itakuwa hivyo hivyo kwa Neymar. Ni rafiki yangu mkubwa, lakini hiyo haitakuwa hivyo katika mechi dhidi ya Real Madrid,” alisema Marcelo.
Marcelo alikataa kuongea lolote kuhusu uhamisho uliokwama wa staa wa Tottenham, Gareth Bale kwa madai kwamba anapenda kuwazungumzia zaidi wachezaji waliopo.

Victor Wanyama amroga bosi Southampton


  Victor Wanyama.

Wanyama, Mkenya wa kwanza kucheza ligi hiyo, wikiendi iliyopita alicheza kwa dakika zote 90 katika mechi ya fungua dimba ya msimu mpya dhidi ya West Bromwich Albion ambapo timu yake ilishinda bao 1-0.

NI kama amerogwa. Kocha wa klabu ya Southampton ya Ligi Kuu England, Mauricio Pochettino, amekiri kuwa anatarajia makubwa kutoka kwa Mkenya, Victor Wanyama, ambaye wikiendi iliyopita alianza kuonyesha makali yake kwenye ligi hiyo maarufu katika anga la soka duniani.
Wanyama, Mkenya wa kwanza kucheza ligi hiyo, wikiendi iliyopita alicheza kwa dakika zote 90 katika mechi ya fungua dimba ya msimu mpya dhidi ya West Bromwich Albion ambapo timu yake ilishinda bao 1-0.
Baada ya kumpanga Mkenya huyo na kumfuatilia kwa makini uwanjani, kocha huyo ameiambia tovuti ya klabu hiyo akisema: “Wanyama ameonyesha kiwango kikubwa, ni mechi yake ya kwanza lakini ameonyesha na kwa kiasi gani mchango wake utahitajiwa msimu huu.
“Amekuwa na ushirikiano mzuri na wenzake na hiki ndicho kitu kilichotufanya tumsajili. Huu ni mwanzo naamini mambo yataongezeka kuwa mazuri.”
Kiungo huyo ambaye pia nahodha wa Harambee Stars, katika mechi hiyo alikuwa nguzo muhimu akikumbushia enzi zake alipokuwa Celtic ya Scotland.
Bao la ushindi la timu yake lilifungwa na Rickie Lambert katika dakika ya mwishoni.

Siri za mkataba wa Ngassa na Simba zafichuka rasmi


Mrisho Ngassa  

  WAKATI Mrisho Ngassa amepitishwa kuichezea Yanga msimu ujao wa Ligi Kuu Bara, imedhihirika kuwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) liliupokea mkataba wa Simba tangu Desemba 17, mwaka jana.
Habari kwa Vina imeuona mkataba wa Simba na Ngassa, ambao umegongwa muhuri wa TFF kuonyesha kuwa ulipokelewa katika shirikisho hilo tangu Desemba 17 mwaka jana.
Mkataba huo, unaonyesha kuwa Ngassa alisaini kuichezea Simba Agosti 2, mwaka jana na kwamba ulitakiwa uanze kutumika Mei 22 mwaka huu na kumalizika Mei 31 mwakani.
Katika moja ya makubaliano kwenye mkataba huo, Ngassa haruhusiwi kuichezea Yanga katika kipindi hicho au timu nyingine yoyote na mshahara wake ungekuwa Sh2 milioni kwa mwezi.
Hata hivyo katika kikao chake cha mwishoni mwa wiki, Kamati ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Soka (TFF), chini ya Alex Mgongolowa ilimuidhinisha Ngassa kuchezea Yanga, lakini ikamfungia mechi sita pamoja na kumtaka arejeshe Sh30 milioni ambazo alichukua Simba pamoja na asilimia hamsini ya fidia ambazo ni Sh15 milioni.
Kamati hiyo ilibaini kuwa Ngasa alisaini mkataba mwingine Simba (katika kipindi ambacho alikuwa na mkataba na Azam) na anatakiwa kurejesha fedha alizopokea Msimbazi Sh30 milioni pamoja na fidia ya asilimia 50 (Sh15 milioni) ya fedha hizo hivyo kufanya awe anadaiwa Sh 45 milioni.
Kamati hiyo pia imemfungia mechi sita za mashindano (kuanzia mechi ya Ngao ya Jamii Jumamosi iliyopita), na anatakiwa awe amelipa fedha hizo ndani ya kipindi hicho cha kukosa mechi hizo. Akishindwa, hataruhusiwa kucheza hadi atakapolipa fedha hizo.
Hiyo ina maana kuwa Ngassa amekosa mechi ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam na nyingine tano za Ligi Kuu Bara ambazo ni dhidi ya Ashanti, Coastal Union, Mbeya City, Prisons na Azam.
Kwa mara ya kwanza, Ngassa ataonekana katika Ligi Kuu Bara, Yanga itakapocheza dhidi ya Ruvu Shooting Septemba 28 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

JK ataka vyuo vikuu nchini kudahili wanafunzi wengi


            Rais Jakaya Kikwete

Dar es Salaam. Rais Jakaya Kikwete amevitaka vyuo vikuu nchini kuweka nguvu zaidi, kuhakikisha vinadahili wanafunzi wa shahada za juu ili kupata wahadhiri.
Akizungumza baada ya kutoa hati idhini kwa Vyuo Vikuu na Vyuo Vikuu Vishiriki vinane, Rais Kikwete alisema kufanya hivyo vitakabiliana na tatizo la uhaba wa wahadhiri linalovikabili hivi sasa.
“Pale kwenye upungufu tusisite kutafuta wataalamu wengine kutoka nje ya nchi. Wakati wa miaka ya 1970 tulipokuwa tunasoma pale Chuo Kikuu (Mlimani), tulikuwa na wahadhiri wengi kutoka nje,” alisema Rais Kikwete.
Licha ya suala hilo, Rais Kikwete alisisitiza umuhimu wa vyuo hivyo kuwekeza kwenye utoaji elimu bora.
“Ikumbukwe idadi kubwa ya wanafunzi haitoshi, lazima tuzingatie ubora. Tunataka mwanafunzi anayepata shahada nchini ajulikane popote anapokwenda,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:
“Isiwe shahada ya kibongobongo, akifika nje anaonekana kama ana stashahada.”
Pia, alisema kuna changamoto kubwa ya upatikanaji wa wanafunzi wa kutosha kujiunga na vyuo vikuu.
Alisema nafasi za vyuo vikuu kwa mwaka ni zaidi ya 78,000, lakini wanaopatikana ni 43,000, changamoto ambayo lazima wakabiliane nayo.
Alisema idadi ya wanafunzi wanaojiunga na vyuo vikuu nchini ni ndogo, ikilinganishwa na wanaojiunga na taasisi hizo kwa nchi nyingine.
Rais Kikwete aliiagiza Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuhakikisha inatekeleza kwa ufanisi, mpango wa Matokeo Makubwa Sasa ( Big Result Now). Alivitaka vyuo hivyo kuhakikisha vinajitafutia njia nyingine za mapato, badala ya kusubiri karo.
Vyuo vilivyopata Hati Idhini ni Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira (Tuma), Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Tanzania (Saut) na Chuo Kikuu Kishiriki cha Ruaha (Ruco). Vingine ni Chuo Kikuu cha Mount Meru (MMU), Chuo Kikuu cha Arusha (UOA), Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini Dar es Salaam (Tudarco), Taasisi ya Afrika ya Nelson Mandela ya Sayansi na Teknolojia, Arusha (NM-AIST) na Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (Must).

Mwakyembe awashukia wapelelezi dawa za kulevya!


Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe  


Dar es Salaam. Waziri wa Uchukuzi, Dk Harrison Mwakyembe amewashukia waendesha mashitaka na wapelelezi kesi zinazohusiana na dawa za kulevya kuwa hadi sasa zimefikia 36 lakini hakuna taarifa zake.
Mwakyembe aliyasema hayo wakati akizungumza kwenye Kipindi cha Jenerali On Monday kilichorushwa na Kituo cha Televisheni cha Channel Ten juzi usiku.
Mwananchi iliwasiliana na Mkurugenzi wa Mashtaka, Elieza Feleshi kuhusiana na hilo, lakini hata hivyo simu yake ilikuwa haipatikani. Hata ilipofika ofisini kwake, ilielezwa kuwa alikuwa kwenye mkutano.
Kamanda wa Kikosi cha Kuzuia Dawa za Kulevya, Godfrey Nzowa alipotafutwa jana kuzungumzia hali hiyo, simu yake ilikuwa haipatikani.
“Kila anayekamatwa lazima achukuliwe hatua stahiki kwa kosa lake na hakuna sababu ya kuleana wala kuogopana,” alisema Dk Mwakyembe ambaye ametangaza kujitoa muhanga kupambana na mtandao wa dawa za kulevya nchini.
Mwakyembe aliyekuwa akizungumzia mapambano hayo aliyoyaanzisha ya dawa za kulevya, alirejea sakata la kuvushwa dawa za kulevya Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, JNIA alisema: “Wote tumewafukuza kazi kwa sababu walihusika kupitisha dawa hizo.”
Hata hivyo, Mkurungenzi wa JNIA, Moses Malaki akizungumza na gazeti hili, alisema juzi kuwa utaratibu wa kuwapatia barua zao umekamilika na sasa kinachofuata ni utaratibu wa kuunda tume ambao utafanyika wakati wowote kwa ajili ya uchunguzi na kuwahoji.
Wafanyakazi hao wa JNIA, wanatuhumiwa kula njama za kupitisha kilo 150 za dawa za kulevya aina ya Crystal Methamphetamine.
Dk Mwakyembe alisema pia kuwa watu hao watafukuzwa kazi pamoja na wahusika wengine. “Ule mkanda unaonyesha watu walivyokuwa wakihangaika siku ile pale. Kuna askari anaonekana anasaidia kupitisha mizigo kwenye mashine, huyu askari ni kazi yake hii?
“Wapo watu walikuwa wakihangaika huku na huko, yaani walikuwa hawatulii, ni kama sinema, wengine wako ‘bize’ na simu badala ya kufanya ukaguzi, sasa tumewafukuza...Najua wapo wengine, nasema kama mtu aliona, alisikia na hakusema naye atakwenda na maji.
Alisema amewasiliana na Waziri wa Mambo ya Ndani, Dk Emmanuel Nchimbi kwa ajili ya kufanikisha kazi hiyo. “Nimemwomba Waziri wa Mambo ya Ndani tufanye kazi na lazima tuumalize huu mtandao.”
Akizungumzia ukaguzi wa mizigo, Dk Mwakyembe alisema lazima mizigo yote ikaguliwe hata bandarini. “Pale Uwanja wa Ndege kuna mitambo pengine bora zaidi kuliko mahala pengine popote Afrika na kama haitoshi, tuongeze mingine zaidi.

Alipoulizwa kama atakuwa na ubavu wa kuzuia ‘unga’ wa vigogo, Mwakyembe alisema: “Kigogo yeyote atakayejitokeza nitamkamata tu...Ajitokeze sasa hivi aone. Nimeshangazwa na kilo 180 kupita, huu mtandao wa kipuuzi lazima kuuvunja.
“Asije mtu akatarajia kuchekewa, ataondoka. Atakayeruhusu mtu kupita na dawa za kulevya, tukibaini, ataondoka tu. Wako wengi wanatafuta kazi. Tulijiachia vya kutosha, na sasa basi.”
Akizungumzia hali ilivyo Bandarini kwa sasa, alisema wameimarisha udhibiti wa upotevu wa makontena. “Hali kwa sasa ni nzuri, ilikuwa aibu, kila siku makontena yanapotea, tulianzisha utaratibu, kontena likipotea kitengo kizima wanakatwa mishahara kulipia,” alisema.
Alisema pia kumeanzishwa utaratibu wa kukagua mizigo yote inayoingia na kutoka.

Friday, August 9, 2013

THAMANI : Ibrahimovic, Ronaldo watikisa Ulaya

Ibrahimovic                                                      
USAJILI wa wanasoka barani Ulaya umeanza kupamba moto, tumeanza kuona nyota kadhaa wakinaswa.
Wiki hii tumemshuhudia Neymar akinaswa kutoka Santos kwenda Barcelona kwa ada ya Euro 57 milioni, naye Jesuz Navas alihama kutoka Sevilla kwenda Manchester City kwa Pauni 17 milioni.
Huo ni mwanzo tu, huenda tukashuhudia usajili wa fedha nyingi zaidi, lakini je ni nani anayeongoza kwa kusajiliwa kwa fedha nyingi katika historia ya soka? Jibu ni Zlatan Ibrahimovic.
Mchezaji huyo kutoka Sweden ndiye kinara wa fedha nyingi na amehama kwenye klabu saba tangu mwaka 2002 na kufanya jumla ya usajili wake kuwa wa Euro 169.1 milioni.
Ibrahimovic alijiunga na PSG akitokea AC Milan katika dirisha la usajili la msimu uliiopita kwa Euro 23 milioni na hapo ndipo alitimiza klabu saba tangu alipoanza kuhama.
Mchezaji huyo alianza kwa kuondoka Malmo FF kwenda Ajax kwa ada ya Euro 9 milioni mwaka 2002, Juventus ililipa Euro 16 kwa klabu ya Ajax ili kumnasa mwaka 2004, nayo Inter Milan ilimnunua nyota huyo kutoka Juventus kwa Euro 24.8 milion (2006).
Baadaye Barcelona ilimnunua kwa Euro 69.5 milioni kutoka Inter Milan (2009). Usajili huo ulishika namba tatu katika historia ya fedha za usajili duniani. 
Mwaka 2011 aliondoka Barcelona kwenda AC Milan kwa Euro 27 milioni. Lakini Cristiano Ronaldo, aliyehama mara mbili tu kwenye maisha yake ya soka, anashika nafasi ya tano na amesajiliwa kwa jumla ya Euro 111.5 milioni.
Mchezaji huyo alitoka Sporting Lisbon kwenda Man United kisha akaondoka Old Trafford kwenda Real Madrid kwa Euro 94 milioni ukiwa ni usajili mkubwa zaidi kwa mara moja kuwahi kutokea duniani.
Nyota wa Ireland, Robbie Keane, ndiye mchezaji ambaye amehama klabu nyingi zaidi tangu mwaka 1999 ambapo ameibuka kwenye klabu tisa.

BENITEZ (CHUCHO) : Afariki akiacha penzi la sinema la mrembo wake

 Liseth akiwa ameshikilia picha ya mumewe, Benitez katika Uwanja wa Ndege wa Doha



STAA wa Ecuador na klabu ya Jaish ya Qatar, Christian Benitez,  aliyefariki wiki iliyopita, ameondoka duniani akiacha penzi tamu la mrembo, Liseth Chala, ambaye alimuoa katika ndoa ya utata mithili ya filamu ya kusisimua.
Penzi lao lilikuwa maarufu nchini Ecuador, si tu kutokana na umaarufu wao, bali kwa jinsi lilivyokuwa la dhati na ambalo limesababisha simanzi kubwa baada ya kufariki kwa Benitez akiwa Qatar.
Walikutana akiwa na miaka 12
Benitez alimuoa Liseth mwaka 2007. Mrembo huyo ni mmoja kati ya watoto watatu wa staa wa zamani wa Ecuador, Cleber Chala, 42, ambaye alistaafu soka mwaka 2008.
Wakati wakikutana, Liseth ambaye kwa sasa ana umri wa miaka 23, alikuwa na miaka 12 tu. Wakati huo Benitez alikuwa na umri wa miaka 17 akichezea klabu ya Nacional ambayo pia baba yake Liseth, Kleber alikuwa akichezea.
Kutokana na hali hiyo, Cleber alikataa mwanaye asiwe na uhusiano na Benitez kutokana na umri wao kuwa mdogo na akampiga marufuku asimuone na binti yake popote pale iwe nyumbani au uwanjani.
Hata hivyo, Benitez ambaye baba yake mzazi, Ermen pia alikuwa mwanasoka maarufu nchini Ecuador aliendelea kubisha na katika hali ya kushangaza Benitez na Liseth walipanga mipango ya ndoa ya siri ingawa wazazi wao walianza kuwashitukia moja kwa moja.
Baada ya maongezi ya muda mrefu kati ya Benitez na Cleber, mwishowe Cleber aliondoa ugumu na kumruhusu Benitez kumuoa binti yake katika harusi ya bomani iliyofanyika nchini Ecuador Julai 2006. Wakati huo Liseth alikuwa na umri wa miaka 15 tu.
Hata hivyo, Benitez na Lisa walipewa sharti moja la kila mmoja kuendelea kuishi na wazazi wake. Wakati huo, baba yake Liseth alikuwa na umri wa miaka 35 tu, huku Benitez akiwa na umri wa miaka 20.
Kwa kuwa wote wawili walikuwa wanasoka mahiri, ghafla wakajikuta wakiwa marafiki. Mama yake Liseth alijikuta mwenye furaha baada ya kuongezeka kwa Benitez katika familia yao.
Liseth hakukacha shule baada ya kuolewa akiwa na umri wa miaka 15 tu. Aliendelea na maisha yake huku akisoma katika shule ya Colegio Lesval.

Hata hivyo aliweka wazi kwamba angeacha kuishi nyumbani na kwenda nje ya nchi kama Benitez angepata timu nje ya Ecuador.
Ndicho kilichofuata. Julai 2006 wakati Benitez aliposajiliwa na klabu ya Santos Laguna ya Ligi Kuu Mexico, Liseth alitimka nyumbani kwenda naye Mexico.
Hata hivyo, kabla ya kuondoka, walifunga rasmi ndoa ya kanisani katika eneo la Iglesia Guapulo mji mkuu wa Quito, Ecuador, wakati huo Liseth alikuwa na miaka 17.
Aliingia kanisani akitembea kwa madaha huku akiwa ameuegemea mkono wa baba yake mzazi.
Ampiga mkwara mumewe, nchi yafurahi
Liseth alipata watoto watatu na Benitez. Wawili kati ya hao ni pacha Roger Cristiano na Emily Guadalupe ambao aliwazaa akiwa na umri wa miaka 18, ilikuwa Agosti 10, 2009 katika Hospitali ya De la Mujer mjini Torreon, Mexico.
Katika pambano moja muhimu la timu ya taifa lake la Ecuador dhidi ya Colombia, Liseth akiwa na mimba ya miezi mitatu alisikika akimwambia mumewe: “Kama haufungi bao, usirudi hapa nyumbani.”
Siku iliyofuata magazeti yote nchini Ecuador yaliandika kichwa hicho cha habari. Benitez na wenzake walicheza soka maridadi na kuichapa Colombia huku Benitez mwenyewe akifunga bao moja na hivyo kuruhusiwa kurudi nyumbani baada ya mechi. Liseth alijifungua mtoto wa kike Desemba 12, 2012.
Benitez amfia Liseth mikononi
Baada ya kukipiga katika klabu ya Laguna, Benitez alienda kwa mkopo katika klabu ya Birmingham katika msimu wa 2009/ 2010, lakini mwisho wa msimu timu hizo mbili zikashindwa kuafikiana uhamisho wa kudumu na kumfanya Benitez arudi tena Mexico na Liseth.
Mwaka 2011, Benitez alirudi Ecuador na kuiwezesha klabu ya America kutwaa ubingwa wa Ecuador. Hata hivyo, msimu huu alipata dili ya kukipiga katika klabu ya Jaish nchini Qatar na huko ndipo mauti yalipomkuta.
Wiki iliyopita, Julai 28, Benitez aliichezea Jaish mechi ya kwanza akiingia dakika 10 za mwisho dhidi ya Qatar FC. Siku iliyofuata, Benitez alitoka ‘out’ akiwa na Liseth pamoja na watoto kwenda kula katika hoteli moja ya Qatar.

 Ghafla akaanza kusikia maumivu makali ya tumbo na kulalamika. Liseth alimpeleka hospitali moja ya Doha na saa chache baadaye akaanza kukosa hewa na kupumua kwa shida. Baada ya muda alitangazwa kuwa amekufa kutokana na matatizo ya moyo.
Kuna lawama kwamba Benitez hakuwa amepata matibabu timilifu mara baada ya kuwasili. Liseth alimpigia simu baba yake kumfahamisha kuhusu kifo hicho alfajiri ya Julai 29.
Kuzikwa Alhamisi Ecuador
Mwili wake ulisafirishwa juzi Jumapili kwenda mji mkuu wa Ecuador, Quito huku Liseth akiwa bega kwa bega na serikali ya Qatar ambayo kwa kushirikiana na klabu ya Jaish walikodi ndege ya kwenda Ecuador.
Mwili wa Benitez unatarajiwa kuagwa kwa heshima katika ukumbi unaochukua watu 16,000.
Mazishi yake yanatazamiwa kufanyika katika makaburi ya Monte Olivo ambayo yapo karibu na makazi ya timu ya taifa ya Ecuador.
Maelfu ya mashabiki, viongozi wa serikali, wachezaji wenzake, wanafamilia wanatazamiwa kuhudhuria mazishi hayo.
Liseth ambaye ni mpenzi wake wa moyoni tangu akiwa na umri wa miaka 12, anatazamiwa kuwaongoza watoto wake watatu kuweka udongo katika kaburi la mumewe ambaye ametoka naye mbali kimaisha.
Valencia ahudhuria, jezi yake yastaafishwa
Winga mahiri wa Manchester United, Antonio Valencia,  alikuwapo wakati wa kupokea mwili wa Benitez baada ya kuomba ruhusa kutoka kwa kocha wake, David Moyes.
Wawili hao walikuwa wachezaji tegemeo zaidi kwa Ecuador. Shirikisho la Soka la Ecuador pia limeamua kuistaafisha jezi namba 11 ya timu ya taifa hilo iliyokuwa inatumiwa na Benitez.

Jambazi sugu la ATM lanaswa Dar es Salaam

Raia wa Bulgaria akiwa chini ya Ulinzi baada ya kupata kichapo kwa kudaiwa kuiba fedha kwenye mashine ya kutolea fedha (ATM) ya BOA tawi la Mbezi Beach, jijini Dar es Salaam jana.           


     Msako wa wezi wa kwenye Mashine za Kutolea Fedha (ATM), umeanza kuzaa matunda baada ya raia wa Bulgaria kukamatwa akiiba kwenye ATM ya Bank of Africa (BOA), Tawi la Afrikana, Kinondoni, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa taarifa za benki, mtuhumiwa huyo ambaye hakutajwa jina lake alikamatwa baada ya kamera maalumu zilizowekwa kwenye ATM za BOA, kumtambua kuwa ni mwizi sugu wa benki hiyo anayetafutwa.
Mmoja wa wafanyakazi wa benki hiyo ambaye hakupenda kutajwa jina kwa kuwa si msemaji, alisema tukio hilo lilitokea jana saa 12 asubuhi baada ya mtuhumiwa huyo kuwekewa mitambo maalumu ya kumnasa.
Alisema benki hiyo ilipelekewa malalamiko na baadhi ya wateja kwamba wakienda kutoa fedha kwenye ATM wanakuta akaunti zao hazina salio wakati wanaamini zilikuwa na fedha.
Chanzo hicho cha habari kilidai kuwa baada ya kupelekewa malalamiko hayo, waliweka mitambo maalumu ya kuwawezesha walinzi wa maeneo ya ATM za BOA kumbaini mtu atakayetoa fedha kwa njia ya wizi.
“Kama Benki tuliweka mtambo maalumu na mtuhumiwa huyo alionekana kwenye mtambo wetu, hivyo tuliwaagiza walinzi wetu watakapomwona mtu huyo wamkamate haraka sana,”alisema.
Alisema mtuhumiwa huyo alianza mchezo huo kwa muda mrefu ambapo kwa kutumia kadi za ATM zisizojulikana idadi yake, alikuwa anakwenda kwenye ATM mbalimbali za benki hiyo na kutoa fedha hadi Sh10 milioni.
Kuhusu tukio la jana, mmoja wa walinzi wa BOA aliyejitambulisha kwa jina moja la Frenky alisema mtuhumiwa huyo alipofika kwenye ATM hiyo aliingia na kuchukua fedha ambazo alizipeleka kwenye gari lake. Frenky alisema baada ya kupeleka fedha hizo, alirudi kwa mara ya pili ili achukue fedha nyingine ndipo walinzi hao walimkamata na kumfunga pingu.
“Huyu mtuhumiwa mwenye asili ya Kiarabu alifika na gari lake saa 12 asubuhi, aliingia kwenye ATM na kutoa fedha ambazo hazikujulikana ni shilingi ngapi na kuzipeleka kwenye gari lake, baadaye alirejea tena kwa ajili ya kutoa fedha zingine, wakati anaingia ndipo alipokamatwa na mlinzi aliyekuwa analinda hapo,” alisema Frenky.
Kamanda wa Polisi Kinondoni, Camilius Wambura alikiri kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mtuhumiwa anashikiliwa na jeshi hilo huku uchunguzi dhidi yake ukiendelea.
“Ni kweli taarifa nimezipata, mtuhumiwa amekamatwa, bado hatujajua ni kiasi gani ambacho ameiba kwa kutumia mtandao, tunaendelea na uchunguzi,” alisema Wambura.
Tukio kama hili lilishawahi kutokea mkoani Mwanza Februari 19 mwaka huu na Jeshi la Polisi mkoani Mwanza kwa kushirikiana na maofisa ya Benki ya NMB liliwatia mbaroni watu watatu ambao walidaiwa kuiba kiasi cha Sh700 milioni kwa nyakati tofauti. 
    Kaimu Kamanda wa Jeshi la Polisi, Christopher Fuime alisema watuhumiwa hao walinaswa baada ya kuwekewa mtego na maofisa wa benki na polisi saa 6 usiku wa Februari 19, mwaka huu na mtuhumiwa mmoja alibambwa akichukua fedha kwenye ATM ya NMB kwenye Tawi la PPF Plaza Mwanza.
Vifaa walivyokutwa navyo ni kadi bandia 194 za kuchukulia fedha katika ATM za NMB na kati yake kadi 95 zilikuwa na namba 0225152975 zilizotumia namba ya akaunti ya 2258103695 zenye jina na picha ya mtu anayedaiwa kuwa ni Moley L.P.
Kadi nyingine 99 zilikuwa na namba 0506056317 za akaunti namba 5068000322 zikitumia jina moja la Mnuo Z.E na picha moja.
Mbali na kadi hizo waliweza kunasa kadi 36 za Benki ya DTB ambazo kati yake kadi 18 zilikuwa na jina moja la Kelvini G Gratias na namba 20497883, kadi 12 zilitumika jina la J.Paul zenye akaunti namba 2049783 huku kadi sita zikitumia jina moja la Joseph Donald akaunti namba 2049783.
Kadi nyingine tatu zenye maandishi ya Download list na nyingine ikiwa ni kadi ya Visa ya Benki ya KCB yenye namba 413546040003827 zilitumia jina la Elikana Zacharia.

Thursday, August 1, 2013

Serikali yatangaza wanaokwenda ualimu

                                                                                                                                   

        
Dar es Salaam. Serikali imetangaza majina ya wanafunzi 18,754 waliochaguliwa kujiunga na vyuo vya ualimu vilivyo chini yake ikiwa ni ongezeko la wanafunzi 1,659 ikilinganishwa na 17,095 waliochaguliwa mwaka jana.
Kati ya wanafunzi hao, 11,806 wamechaguliwa kusomea ngazi ya cheti (Grade A) na 6,948 watasoma katika ngazi ya stashahada.
Wanafunzi 363 wamechaguliwa kusoma elimu maalumu kwa ngazi ya cheti huku 57 wakisoma elimu hiyo kwa ngazi ya stashahada.
Akizungumza na mwandishi wetu jana, Msemaji wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Ntambi Bunyazu alisema wanafunzi wanatakiwa kuripoti kwenye vyuo walivyopangiwa kuanzia Agosti 15, mwaka huu.
“Usajili utafungwa Agosti 25 saa 12:00 jioni, ‘Joining instructions’ (fomu ya maelekezo ya kujiunga) zitatumwa kwa wahusika kupitia anuani zao.... fomu hizi pia zinapatikana kwenye tovuti ya Wizara ya Elimu na mafunzo ya Ufundi,” alisema.
Taarifa ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi iliyotolewa baadaye jana ilisema kuwa wanafunzi waliochaguliwa wanatakiwa kufika vyuoni wakiwa na vyeti halisi vya kidato cha nne na cha sita vinavyotolewa na Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) , ada ya muhula wa kwanza Sh100,000 au Sh200,000 kwa mwaka.
Wanatakiwa kuwa na “Sare ya chuo kulingana na maelekezo ya chuo husika, fedha za tahadhari chuoni na matumizi binafsi,” inasema taarifa hiyo.
Taarifa hiyo inaeleza pia kuwa wakuu wa vyuo wanatakiwa kuhakikisha wanafunzi wanaosajiliwa ni wale waliopo kwenye orodha iliyotolewa na wizara na si vinginevyo.
Wengi wa wanafunzi hawa ni wale waliohitimu kidato cha nne mwaka 2012 na kidato cha sita mwaka huu. Kwa upande wa wale wa kidato cha nne, matokeo yaliyotangazwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi yalionyesha kuwa watahiniwa 159,609 wa shule walifaulu kwa daraja la kwanza mpaka la nne.
Inaonyesha pia kuwa kwa upande wa Tanzania Bara, wanafunzi 34,599 walifaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu na kati yake waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ufundi walikuwa ni 34,213.
Kwa upande wa matokeo ya kidato cha sita mwaka huu, watahiniwa waliofaulu mtihani huo walikuwa ni 44,366 kati yao 40,242 wakiwa ni wa shule. Matokeo hayo yanaonyesha pia kuwa, watahiniwa 35,880 ndiyo waliofaulu kwa daraja la kwanza mpaka la tatu.
Kwa mujibu wa Kitabu cha Takwimu cha Wizara ya Elimu (Best), mwaka 2012 wanafunzi 17,095 walichaguliwa kujiunga na vyuo mbalimbali vya ualimu nchini.
Kutokana na takwimu hizo, kuna uwezekano mkubwa kwamba wanaokwenda kusoma ngazi ya cheti wanatoka kwenye kundi la wanafunzi waliopata daraja la nne.
Wanafunzi waliopata daraja la nne kwenye mtihani wa kidato cha nne mwaka jana ni 124,260.
Baada ya kutangaza majina ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano pamoja na vyuo vya ufundi, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo aliliambia gazeti hili kuwa wanafunzi waliopata daraja la nne katika kiwango cha alama 27 watachaguliwa kujiunga na vyuo vya ualimu endapo wataomba.
“Vigezo vya kujiunga na kidato cha tano na vile vya vyuo vya ualimu ni tofauti. Kidato cha tano mwisho anatakiwa mtu mwenye alama 25 na masomo yake matatu yawe sawa, ualimu ni alama 27.
“Mwanzoni walikuwa wanakwenda wenye alama 28, lakini mwaka jana tukasema hapana, iwe alama 27 na tutachukua kuanzia waliomaliza shule mwaka 2008 kama wataomba, kwa sasa hivi watu wanaendelea na kazi ya kuwachagua,” alisema Mulugo.
Kwa muda mrefu, wadau wa elimu wamekuwa wakipiga kelele kuhusu wanafunzi wanaochaguliwa kusomea ualimu nchini wakitaka nafasi hiyo ichukuliwe na wale wanaofanya vizuri kwenye masomo yao.

           

Saturday, June 15, 2013

Uganda - Tutatoza Ushuru pesa za Mobile

Uganda imetangaza kuweka kodi ya 10% kwa pesa zote zinazotumwa kwa njia ya simu na mbinu zingine za kutuma pesa.
Mganda akipiga simu
Hii itaathiri pesa zinazotumwa na Waganda waishio nchi za ng'ambo. Waziri wa fedha Maria Kiwanuka pia amesema kuwa anapanga kukusanya zaidi ya $16.5m (£10.6) kwa kutoza kodi simu zote za kimataifa kutoka nchini humo.
Bi Kiwanuka alilazimika kutafuta mbinu ya kuziba pengo la $214m katika bajeti ya serikali ya Uganda, baada ya wafadhili kupunguza msaada wao kwa Uganda kufuatia madai ya ufisadi.
Mwandishi wa BBC mjini Kampala , anasema kuwa wengi wanahofia kuwa bajeti hii, iliyosomwa Alhamisi, inawalemea zaidi watu maskini katika jamii.
Waziri Kiwanuka aliambia bunge kuwa zaidi ya $767m zilizokusanywa na serikali mwaka uliopita zilitoka kwa Waganda waishio ngambo.
Kwa mujibu wa gazeti huru nchini Uganda, Daily Monitor, ushuru huo mpya unaotozwa pesa zinazotumwa kwa simu za mkononi utaathiri zaidi ya watumiaji 8.9m wanaotumia mitandao sita ya simu nchini Uganda.

Serikali inahitaji fedha zaidi

Imeripoti pia kuwa serikali inanuia kukusanya takriban $12m kwa mwaka.
Huduma hii ya kutuma pesa kwa njia ya simu ni maarufu sana nchini Uganda ikizingatiwa kuwa raia wengi wa nchi hiyo hawana akaunti za benki.
Huhduma hii hutumiwa kuwatumia jamaa pesa nyumbani au hata kulipia madeni.

Hii bajeti sio juu ya kuweka kodi mpya, ni kukusanya tu kile ambacho hakijachukuliwa kwa muda, alisema waziri huyo.
Kwa upande wake David Holliday, mkurugenzi mtendaji wa wa shirika la mawasiliano la Telecom, kodi hii mpya bila shaka itaongeza gharama ya matumizi ya simu.
'' pesa kwenye simu imekuwa hali ya maisha ya wananchi wetu kwasababu inamaanisha kuwa hawana haja tena ya kubeba pesa taslimu.
Hata wale ambao hawakuweka pesa zao Benki sasa waliweza kuhifadhi kwenye simu zao kwasababu ni rahisi na bei nafuu'' gazeti la Daily monitor limemnukuu.

Naye Bi Kiwanuka anasema kuwa lengo la bajeti hiyo ni kuwanasa wale ambao hukwepa kulipa kodi na kuishinikiza halmashauri ya ukusanyaji ushuru kufikia malengo ya kodi ya serikali kamilifu.
Waziri wa fedha wa Uganda, Maria Kiwanuka






Wachezaji wa Super Eagles wagoma

Wachezaji wa Nigeria wameshindwa kusafiri kuelekea Brazil kufuatia mzozo kuhusu malipo ya ziada ya wachezaji.
Wachezaji wa Nigeria
Timu hiyo ya Super Eagles, inatarajiwa kucheza mechi yake ya kwanza siku ya Jumatatu, lakini wamesalia nchini Namibia baada ya mechi yao ya kufuzu kwa kombe la Dunia.
Wachezaji wa Nigeria, hawajafurahishwa na uamuzi wa kuwapa dola elfu mbili kila mmoja, baada ya timu hiyo kutoka sare ya kufungana bao moja kwa moja na Namibia mjini Windhoek.
Wachezaji hao wamesisitiza kuwa shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria ni sharfti iongeze fedha hizo maradufu kabla ya wao kusafiri.
Ripoti zinasema kuwa wachezaji hao wamesema kuwa hawawezi kusafiri kuelekea Brazil hadi mzozo huo utakapotatuliwa.
Kuna wasi wasi kuwa mabingwa hao wa Afrika huenda wakakosa kushiriki katika fainali za kombe la shirikisho, itakayo anza tarehe kumi na tano hadi tarehe thelathini mwezi huu.
Rais wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Nigeria NFF, Aminu Maigari, alifanya mazungumzo na wachezaji hao jana usiku mjini Windhoek, kuwaeleza kuwa shirikisho lake halina fedha na ndio sababu malipo hayo ya ziada yalipunguzwa.

Wiki iliyopita, vyombo vya habari nchini Nigeria, viliripoti kuwa wachezaji hao walizozana na maafisa hao wa NFF mjini Nairobi kuhusiana na malipo ya ziada baada ya Super Eagles kuilanza Harambee Stars bao moja kwa bila.
Wachezaji hao walitaka kulipwa dola elfu kumi kila mmoja kufuatia ushindi huo, lakini maafisa hao wa NFF walikataa pendekezo hilo.
NFF ambayo kwa sasa inakabiliwa na matatizo ya kifedha imelazimika kupunguza matumizi yake, likisema lilitumia kiasi kikubwa cha fedha zake katika fainali za kuwania kombe la mataifa ya Afrika iliyoandliwa nchini Afrika Kusini.
Nigeria ilikuwa imetangaza kuwa huenda ikajiondoa kwenye michuano ya kuwania kombe la mataifa ya Afrika kwa wachezaji wanaoshiriki ligi ya nyumbani CHAN kutokana na matatizo ya kifedha.
Lakini uamuzi huo ulifutiliwa mbali baada ya serikali ya nchi hiyo kuingilia kati.

Wachezaji hao walitarajiwa kusafiri hadi Johannesburd leo kabla ya kuelekea nchini Brazil.


Kocha wa Nigeria








Watoto 93,000 wameuawa Syria

Umoja wa Mataifa umesema takriban watoto elfu tisini na tatu wameuawa nchini Syria tangu kuanza kwa mapigano nchini humo.
Makaburi ya watu waliouawa nchini Syria
Kwa mujibu wa takwimu hizo, idadi hiyo imeongezeka kwa zaidi ya elfu thelathini, tangu umoja huo ulipotoa takwimu zake Januari mwaka huu.
Ripoti hiyo imesema kuwa watu elfu tano hufa nchini Syria kila mwezi tangu Julai mwaka uliopita
Hata hivyo takwimu hizo huenda sio idadi kamili na Umoja wa Mataifa umesema huenda idadi ya waliouawa huenda ikawa kubwa zaidi, kwa kuwa vifo vingi havijaripotiwa.
Asilimia themanini ya waliouawa ni wanaume, lakini Umoja huo umeongeza kusema kuwa tayari umethibitisha kutokea kwa vifo vya zaidi ya watoto elfu moja mia saba ambao wako chini ya umri wa miaka kumi.
Vile vile, kuna ripoti kuwa watoto wengine waliteswa kabla ya kuuawa kinyama.
Afisa mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na masuala ya haki za binadam Navi Pilllay, amesema wamepokea ripoti ya kutokea kwa mauaji ya familia nyingi wakiwa na watoto wao, ishara kuwa vita vinavyoendelea nchini Syria vimegeuka kuwa janga kuu huku maelfu ya watu wakiendelea kuuawa kila siku.
Wakati huo huo, wanaharakati wa upinzani nchini Syria na shirika la habari la serikali wamesema kuwa makombora yaliyorushwa na wanajeshi wa waasi yameanguka katika uwanja mkuu wa ndege mjini Damascus.
Moja ya makombora hayo yaliyotengenezwa nyumbani, lilianguka karibu na barabara ya kurukia ndege na hivyo kulazimisha safari kadhaa za ndege kucheleweshwa kwa sababu za kiusalama.
Shambulio hilo ndilo la kwanza katika uwanja huo wa ndege ambao kwa sasa umezingirwa na wanajeshi wa serikali.

Fastjet kutoa huduma za bei nafuu

Shirika la ndege, linalotoa huduma za usafiri wa ndege kwa bei nafuu Fastjet, limepata kibali cha kuanzisha safari za ndege za kimataifa za bei nafuu, kutoka Tanzania hadi Afrika Kusini, Zambia na Rwanda.

Ndege ya shirika la EasyJet
Kampuni hiyo inayomilikiwa na Stelios Haji-Ioannou, ambaye ni mmiliki wa shirika la ndege la Easyjet, lililo na makao yake barani ulaya.
Shirika hilo limetangaza kuwa litaanzisha safari za ndege katika mataifa hayo kwa bei nafuu huku abiria wakilipa dola mia moja pekee.
Kwa sasa shirika hilo linahudumia wasafiri nchini Tanzania pekee.
Raia wengi na hasa wafanya biashara wamefurahishwa na tangazo hilo, wakisema kuwa itapunguza gharama za usafiri na hivyo kuimarisha biashara katika kanda hiyo.
Nchini Kenya, shirika la ndege la Kenya Airways ambalo ni moja ya mashirika makubwa ya ndege barani Afrika, limepata pigo kubwa baada ya kupata hasara kubwa katika kipindi cha miaka minne iliyopita.
Ripoti zinasema kuwa shirika hilo lilipata hasara ya zaidi ya dola milioni mia moja kabla ya kutozwa ushuru, kiwango ambacho ndicho mbaya zaidi tangu mwaka wa 2009.
Shirika hilo lilikuwa maarufu sana kwa abiria wanaosafiri magharibi, mashariki, kusini na katika mataifa ya Afrika ya kati.

Afya ya Mzee Mandela imeimarika

Hali ya Afya ya aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Nelson Mandela, inaendelea kuimarika.
Rais wa Afrika Kusini Jacob Zuma, amesema kuwa amefahamishwa na madaktari wanaomtibu kuwa, hali ya Mzee Mandela ambaye anaendelea kupokea matibabu katika hospitali moja mjini Pretoria imeimarika.
Mandela amekuwa akiugua maradhi ya mapafu mara kwa mara

Rais Zuma amesema amefurahishwa na jinsi hali ya rais huyo inavyoendelea kuimarika, baada ya kudhohofika sana siku chache zilizopita.
Siku ya Jumanne rais Zuma, alisema kuwa nchi yote inazidi kumwombea Mzee Nelson Mandela ili apate afueni haraka.
Rais huyo wa zamani amelazwa hospitalini Pretoria, ambako anatibiwa maambukizi ya mapafu.
Katika taarifa yake rais Zuma amesema japokuwa Mandela ameathirika sana, madaktari wanaomshughulikia wanafanya kazi nzuri.
Rais huyo mstaafu wa Afrika Kusini, amelazwa hospitalini kwa siku ya tano leo ambako anapokea matibabu ya ugonjwa wa mapafu.
Duru kutoka kwa ofisi ya rais Jacob Zuma, zinasema kuwa Mandela mwenye umri wa miaka 94, yuko katika hali mbaya ingawa imeweza kudhibitiwa.

Familia ya Mandela

Jamaa zake pamoja na aliyekuwa mkewe Winnie Madikizela-Mandela, walimtembelea hospitalini Jumatatu
Mwanawe Mandela Zenani (Mandela-Dlamini), pia alirejea kutoka nchini Argentina, ambako yeye ni balozi.
Serikali imekuwa ikisema kuwa hali ya Mandela inatia wasiwasi ingawa madaktari wameweza kuidhibiti.
Amekuwa katika chumba ya wagonjwa mahututi tangu kulazwa hospitalini Jumamosi kwa mara ya tatu mwaka huu.
Mwezi Disemba , bwana Mandela alilazwa hospitalini kwa siku 18 baada ya kupata maradhi ya mapafu,
Kumekuwa na taarifa za simanzi kwa mara ya kwanza huku familia yake ikikusanyika kando yake, baadhi ya watu wakisema kuwa ni muda wamwache Mandela aende zake.
Bwana Mandela, mwenye umri wa miaka 94, alipelekwa hospitalini mapema Jumamosi , ikiwa ni mara ya tatu kulazwa hospitalini mwaka huu.
Kwa mujibu wa duru za urais, Mandela amekuwa akiugua kwa muda mjini Johannesburg baada ya kukumbwa tena na ugonjwa wa mapafu.
Msemaji wa serikali Mac Maharaj amesema kuwa maafisa katika hospitali wanataka kudhibiti idadi ya watu wanaozuru hospitali hiyo ili wampunguzie bwana Mandela usumbufu.
Alilazwa hospitalini baada ya hali yake kuwa mbaya zaidi mnamo Jumamosi.
Kwa mujibu wa taarifa za urais, Rais Jacob Zuma, amerejelea wito wake kwa watu nchini Afrika Kusini kumuombea Madiba wakati huu anapougua.
Lakini mwandishi wa BBC mjini Pretoria, Karen Allen, anasema kuwa kuna matumaini madogo kuwa Mandela aliyeongoza vita dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi, huenda akapona.
Anasema kuwa wengi walipata matumani baada ya bintiye Mandela Zindzi, kusema kuwa babake yuko salama na kuwa anaendelea kupata nafuu.
risala za heri njema na afueni kwa rais mstaafu Nelson Mandela
Mkewe Mandela Graca Machel, alifutilia mbali, ziara yake mjini London Jumamosi ili kuwa kando ya mumewe.
Mandela alikuwa Rais wa Afrika Kusini kati ya mwaka 1994 hadi 1999.
Alifungwa jela miaka 27 na anaaminika kuwahi kuugua ugonjwa wa mapafu alipokuwa akifanyishwa kazi ngumu katika machimbo ya mawe akiwa jela.