Instagram

Wednesday, August 21, 2013

Victor Wanyama amroga bosi Southampton


  Victor Wanyama.

Wanyama, Mkenya wa kwanza kucheza ligi hiyo, wikiendi iliyopita alicheza kwa dakika zote 90 katika mechi ya fungua dimba ya msimu mpya dhidi ya West Bromwich Albion ambapo timu yake ilishinda bao 1-0.

NI kama amerogwa. Kocha wa klabu ya Southampton ya Ligi Kuu England, Mauricio Pochettino, amekiri kuwa anatarajia makubwa kutoka kwa Mkenya, Victor Wanyama, ambaye wikiendi iliyopita alianza kuonyesha makali yake kwenye ligi hiyo maarufu katika anga la soka duniani.
Wanyama, Mkenya wa kwanza kucheza ligi hiyo, wikiendi iliyopita alicheza kwa dakika zote 90 katika mechi ya fungua dimba ya msimu mpya dhidi ya West Bromwich Albion ambapo timu yake ilishinda bao 1-0.
Baada ya kumpanga Mkenya huyo na kumfuatilia kwa makini uwanjani, kocha huyo ameiambia tovuti ya klabu hiyo akisema: “Wanyama ameonyesha kiwango kikubwa, ni mechi yake ya kwanza lakini ameonyesha na kwa kiasi gani mchango wake utahitajiwa msimu huu.
“Amekuwa na ushirikiano mzuri na wenzake na hiki ndicho kitu kilichotufanya tumsajili. Huu ni mwanzo naamini mambo yataongezeka kuwa mazuri.”
Kiungo huyo ambaye pia nahodha wa Harambee Stars, katika mechi hiyo alikuwa nguzo muhimu akikumbushia enzi zake alipokuwa Celtic ya Scotland.
Bao la ushindi la timu yake lilifungwa na Rickie Lambert katika dakika ya mwishoni.

0 comments: